Habari Kamili
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) CCM, Jason Rweikiza ametoa punguzo aslimia 40 kwa kila mkazi wa Kata ya Msingwa, Mbezi, Dar es Salaam, atakayepeleaka mototo katika shule yake ya St. Anne Marie iliyopo eneo hilola Kimara.
Rweikiza alitoa ‘ofa’ hizo, baada ya kufungua Ofisi ya CCM tawi la Msingwa katika hafla iliyoambatana na kuwakabidhi bendera za CCM wajumbe 15 wa mashina ya CCM waliochaguliwa katika wa kata hiyo.
"kutokana na kwamba nimekuwa eneo hili na kufanya shughuli zangu hapa na wengi wenu hapani wana-CCM wenzangu, natoa ofa ya punguzo la asilimia 40 ya ada, kwa mzazi wa hapa atakayeleta mototo wake kwenye shule yangu ya St. Anne Marie iliyopo hapa Mbezi”, alisema Rweikiza.
Shule hiyo ya St Anne Marie, inatoa masomo ya shule za awali, msingi, sekondari hadi kidato cha sita.
Pia aliahidi kutoa mchango wa sh. 500,000 kwa ajili yak umalizia ujenzi wa ofisi ya CCM aliyofungua, na kueleza kwamba ofa la punguzo la ada na msaada wa fedha hizo hatoi kwa sababu ya maadalizi ya kugombea ubunge kwa kuwa hana nia ya kuwania nafasi hiyo.
Rweikiza aliwataka wanachama wa CCM kulitumia tawi hilokuzingumza mambo muhimu ya ujenzi wa Chama kwa kufanya vikaovyote vya chama kwamujibu wa Katiba.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269