MKURUGENZI wa Chuo cha Muziki cha London (LCM) cha Chuo Kikuu cha Thames Valley jijini humo nchini Uingrereza, Profesa John Howarad akiwafafanulia jambo, washiriki wa warsha ya uzinduzi wa tawi la chuo hicho Tanzania, jana kwenye ukumbi wa FPCT, Kurasini, Dar es Salaam.
MWENYEKITI wa Tasisi isiyo ya Kiserikali (NGo) ya Human Development Opportunities, ambaye Chuo hicho kitafanyakazi nchini chini ya uratibu wake, Enoy Gwanje akitoa somo kuhusu kuanzishwa kwa utoaji elimu ya shahada hadi ya juu ya muziki kupitia ptogramu zitakazoendeshwa na chuo hicho. Kulia ni baadhi ya waalikwa katika semina ya uzinduzi huo.

Ptofesa Howard (kulia).na mke wa Enoy wakiwa kwenye semina hiyo.

Mtoto Milele Gwanje (4) akifuatilia kwa makini kilichokuwa kikiendelea katika semina hiyo. Mtoto huyo anatarajiwa kufuzu mafunzo ya upigaji kinanda kutoka chuo hicho.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269