Breaking News

Your Ad Spot

Apr 2, 2016

BARAZA LA USALAMA KUTUMA KIKOSI CHA POLISI BURUNDI

Baraza la Usalama kutuma kikosi cha polisi Burundi
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio la kutuma kikosi cha maafisa wa polisi wa umoja huo nchini Burundi kwa lengo la kudhibiti hali ya mambo nchini humo.
Nchi 15 wanachama wa baraza hilo kwa kauli moja zimepasisha rasimu ya azimio iliyoandaliwa na Ufaransa ya kutuma maafisa wa polisi ambao hawajajizatiti kwa silaha kwenda nchini Burundi kudhibiti hali na kuzuia ukiukaji wa haki za binadamu.
Azimio hilo limemtaka Ban Ki-Moon, Katibu Mkuu wa umoja huo kwa ushirikiano na viongozi wa Umoja wa Afrika pamoja na serikali ya Bujumbura kuandaa orodha ya kikosi hicho cha polisi katika muda wa siku 15 zijazo.
Wakati huo huo, Tume Huru ya Kutetea Haki za Binadamu nchini Burundi imeeleza wasi wasi kuhusiana na hali ya kiusalama na kisiasa nchini humo.
Jean-Baptiste Baribonekeza, Mwenyekiti wa tume hiyo amesema watu zaidi ya 380 wamekwishauawa kufikia sasa tangu mgogoro wan chi hiyo uanze Aprili mwaka jana. Baribonekeza amesema hadi kufikia sasa wamepokea kesi 747 za ukandamizaji na ukiukaji wa haki za binadamu tangu mwaka jana 2015. Kadhalika Mwenyekiti wa Tume Huru ya Kutetea Haki za Binadamu nchini Burundi amesema kuwa watu 19 wametekwa nyara wasijulikane waliko na kwamba wengine 27 wamefanyiwa ukatili na dhulma za kutisha wakiwa kizuizini.
Aidha Jean-Baptiste Baribonekeza amefichua kuwa watu zaidi 31,200 wanazuiliwa na vyombo vya usalama nchini humo tangu mwaka jana.
Zaidi ya watu 400 wameripotiwa kuuawa na wengine karibu laki mbili na 40 elfu wamekuwa wakimbizi tangu Burundi ilipotumbukia kwenye machafuko yaliyotokana na Rais Nkurunziza kuamua kugombea tena urais nchini humo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages