Breaking News

Your Ad Spot

Dec 9, 2009

SHEREHE YA MIAKA 48 YA GAZETI LA UHURU, Habari katika Picha

BAADHI ya wafanyakazi na waalikwa wakiwa katika sherehe za miaka 48 ya gazeti laUhuru, Makao Makuu ya kampuni ya Uhuru Publications Ltd, (UPL), mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, juzi. UPL ni washapishaji wa gazeti hilo na Mzalendo na BurudaniBAADHI ya wafanyakazi na waalikwa wakiwa katika sherehe za miaka 48 ya gazeti laUhuru, Makao Makuu ya kampuni ya Uhuru Publications Ltd, (UPL), mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, juzi. UPL ni washapishaji wa gazeti hilo na Mzaalendo na Burudani
MJUMBE wa Bodi ya UPL, Mbunge wa Donge, Ali Ameir Mohammed akimpa cheti cha ufanyakazi bora wa mwaka  2008, Monica Komba,. katika hafla hiyo. Wa pili kulia ni Mhariri Mtendaji wa UPL, Josiah Mufungo

MJUMBE wa Bodi ya UPL, Mbunge wa Donge, Ali Ameir Mohammed akimpa cheti cha ufanyakazi bora wa mwaka huu, Kulwa Magwa,. katika hafla hiyo. Wa pili kulia ni Mhariri Mtendaji wa UPL, Josiah Mufungo


MGENI Rasmi katika hafla hiyo,  Mbunge wa Donge ambaye ni Mjumbe wa Bodi wa UPL, Ali Ameir Mohamed, na  Mhariri Mtendaji wa UPL, Josiah Mufungo wakimsiliza mfanyakazi wa kampuni hiyo, Evas-weet Musiba aliyekuwa akiwaambia jambo. Kulia ni Naibu Mhariri Mtendaji wa UPL, Jacqueline Liana na kushoto ni Kaimu Mhasibu Mkuu wa UPL, Alvera Kabwogi.

BAADHI ya wafanyakazi wakisakata muziki katika sherehe hiyo

MGENI rasmi na viongozi wa UPL wakigonganisha glasi za vinywaji katika hafla hiyo.

MGENI rasmi na Mhariri Mtendaji wa UPL, wakitazama toleo la gazeti la Uhuru, baada ya kuwa tayari kuchapishwa kiasi cha saa tatu usiku wakati sherehe zikiendelea.

MHARIRI Mtendaji wa UPL, Josiah Mufungo (kushoto), Naibu Mhariri Mtendaji, Jacqueline Liana na Meneja Utawala na Utumishi wa UPL, Lucas Kisasa, wakiinua wote glasi za viwanywaji kulityakia gazeti maisha marefu, wakati wa sherehe hiyo.

NAIBU Mhariri Mtendaji wa UPL, Jacqueline Liana, akizungumza na wageni waalikwa, Mhariri Mtendaji wa TSN, Mkumbwa Ally na Mkurugenzi wa Radio Uhuru, Mikidadi Mahmud, wakati wa hafla hiyo.

Wageni waalikuwa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa UPL na mgeni rasmi katika hafla hiyo.

WAFANYAKAZI bora wa mwaka huu na wa mwaka jana, wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi na viongozi wa UPL wakati wa sherehe hiyo.

BAADHI ya wafanyakazi na wagene waalikwa wakisakata muziki wakati wa sherehe hiyo.

MGENI rasmi akimkabidhi cheti cha ufanyakazi Bora, Kaimu Mhasibu Mkuu wa UPL, Alvera Kabwogi, katika sherehe hiyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages