Breaking News

Your Ad Spot

Dec 4, 2010

KILI STARS YAICHANA BURUNDI 2-0 KOMBE LA CHALENJI; YATINGA NUSU FAINALI

 
MSHAMBULIAJI wa Kilimanjaro Stars, Nurudin Bakari (kushoto), akichuana na beki wa  Burundi, Habarugira Paul, timu hizo zilipomenyana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, katika mechi ya Kombe la Chalenji, leo. Stars iliibuka na ushindi wa mabao 2-0. 
Msdhambuliaji wa Kilimanjaro Stars Mrisho Ngassa  akimtoka beki wa  Burundi katika mechi hiyo 
Kipa wa akiba wa  Burundi, akiwa na huzuni kwa timu yake kula kipigo cha mabao 2-0 katika mechi hiyo 
Kutokana na watu kuruhusiwa kuingia bure, Uwanja wa Taifa, ulielemewa wakati wa mechi hiyo, ikalazimu polisi kuwafukuza mashabiki wengine kwa gari la maji ya kuwasha. 
Mashabiki wakitimka kuongopa kumwagiwa maji ya kuwasha 
Stars wakitoka Uwanjani kifua mbele  kutokana na ushindi huo 
Wachezaji wa Amahoro ya Burundi wakiwa wametahayari baada ya mechi 
Mashabiki waliobahatika kuingia uwanjani wakishangilia ushindi

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages