Breaking News

Your Ad Spot

Jan 19, 2011

JK AONGOZA KUAGA/MAZISHI YA JAJI MSTAAFU, DAN MAPIGANO

RAIS Kikwete ameungana na mamia ya waombolezaji wakiwemo ndugu, majaji, mawakili na wafanyakazi mbalimbali wa tasnia ya sheria katika mazishi ya Jaji Mstaafu Dan Mapigano, leo jijini Dar es Salaam.
        Kabla ya mazishi hayo yaliyofanyika kwenye makaburi ya Kinondoni, asubuhi, kwanza  Rais Kikwete aliungana na waombolezaji hao, kuaga mwili, nyumbani kwa marehemu, eneo la Mwenge.
        Baada ya shughuli ya kuaga nyumbani, mwili ulipelekwa katika Kanaisa la Wadventista wa Sabato, Magomeni Mwembechai kwa ajili ya ibada, iliyofanyika kuanzia saa 2.30 hadi saa 3.00 asubuhi.
        Baada ya ibada hiyo, mwili wa marehemu Mapigano ulipelekwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, ambako pia zilifanyika shughuli za kuuaga, kwa waombolezaji kuongozwa na Rais Mstaafu Ali Hassani Mwinyi na Jaji Mkuu Mohammed Chande Othman.
        Shughuli za kuagwa mwili kwenye viwanja hivyo zilitangukiwa na kusomwa wasifu wa marehemu ambao ambao Jaji Kiongozi, Fakih Jundu kwa niaba ya jaji Mkuu Othmani.
        Akisoma wasifu huo, pamojana na sifa kadhaa, Jaji Jundu alisema, Marehemu Jaji mstaafu, Mapigano, aliyezaliwa mwaka 1939, katika kitongoji cha Murangi wilaya ya Musoma Vijijini, baada ya masomo yake ya msingi na sekondari, alijiunga Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, mwaka 1961 kuchukua shahada ya kwanza ya biashara, lakini mwaka 1963 alisitisha masomo hayo ili kusoma shahada ya sheria.

        Mwaka 1963 alijiunga na kitivo cha sheria cha University of London/Dar es Salaam College (Lumumba) na kuhitimu masomo ya shahada ya kwanza ya sheria mwaka 1965.

        Alisema, mwaka 1966 Marehemu Mapigano, aliajiriwa na idara ya Mahakama kuwa Hakimu Mkazi na kwamba katika utumishi wake katika wadhifa huo, alifanya kazi katika maeneo mbalombali ikiwemo mikoa ya Kilimanjaro, Unguja, Pemba, Dar es Salaam.
       Mwaka 1974 aliapishwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, wadhifa amabao alifanya nao kazi katika mikoa mbalimbali kabla ya kustaafu kazi mwaka 1999.
        Mbali ya Rais mstaafu, Ali Hassani Mwinyi, kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Mapigano ambaye alifariki dunia, Jumamosi iliyopita, walikuwepo pia viongozi mashuhuri wakiwemo Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, Waziri wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, Mawaziri wakuu wa zamani, Joseph Warioba na Frederick Sumaye.

1 comment:

  1. If you want great sex, give it and demand it!Don't 'Time' Love. Some people really like to go all out for a special event and if they have enough money or have saved up for a long time, making sure a certain time in their life was going to be celebrated in style, why not get somebody to plan a spectacular party in the ideal location to hold it? Why do they take their most prized young possessions and thwart their long-term development just so they can temporarily have a good 6th-inning reliever? [URL=http://lopolikumibo.com ]cowberries[/URL] The 458 Spider's incredible dynamic behavior is due to its sophisticated multi-link suspension and new generation magnetic shock absorbers, responsive steering rack and control systems. When and if you finally do start to tap into your gift and when you have the courage to do the right thing, instead of not listening and doing what your ego wants; you will begin to experience what it's like to be "Divinely" guided down the right path.

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages