Breaking News

Your Ad Spot

Jan 17, 2011

MRADI WA MCHUCHUMA KUANZA KAZI KABLA YA JK KUMALIZA MUHULA WAKE

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo Tanzania (NDC) linalosimamia mradi huo, Dk. Clisant Mzindakaya, akimtanabahisha jambo kwa undani, Makamu Mwenyekiti wa Kampuni ya China ya  Sichuan Hondga, Liu Canglong, kabla ya kuanza mazungumzo ya maafikiano kuhusu kuanza kwa mradi wa Mawe wa Mchucghuma na wa Chuma wa Liganga, jana mjini Dar es Salaam. 
Wawakilishi wa NDC (kushoto), wakiwa tayari kufanya majadiliao na wawakilkishi wa kampuni ya China ya  Sichuan Hondga, leo katika ukumbi wa DICC mjini Dar es Salaam.
=============================
Akizungumza na waandishi wa Habari, leo kabla ya mazungumzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa NDC,  Gideon Nasari alisema, mazungumzo hayo yatachukua siku nne, na taarifa kuhusu hatma ya mazungumzo ya maafikiano hayo  itatolewa baadaye.
Lakini akadokeza kwamba mradi wa makaa ya mawe unatarajiwa kuanza miezi sita baada ya maafikiano kufikiwa lakini zaidi ya hilo utakamilika kabla ya Rais wa awamu ya nne, Dk. jakaya Kikwete kumaliza muda wake.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages