Breaking News

Your Ad Spot

Jan 3, 2011

MSIBA SIKINDE

AKLIYEKUWAmpi gita zito la bass  wa DDC Mlimani Park Orchestra,Mustafa Ngosha
(pichani) ambaye alijulikana zaidi kwa jina  la Ngosha amefariki dunia ljana baada ya kusumbuliwa na
maradhi kwa muda kidogo.

Ngosha alijiunga na DDC Mlimani Park miaka ya mwanzoni ya 90, akiwa anajulikana kama Charles John Ngosha ila baadae alibadili dini na Kuwa muislam na kupewa jina la Mustafa.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Amana,Ilala jijini Dar es Salaam,

Msiba upo nyumbani kwa marehemu pale Tandale kwa Popobawa  na kwa mujibu wa mmoja wa
wanakamati ya mazishi na mwanamuziki mkongwe Hassan Rehani Bitchuka, taratibu za  mazishi  zinafanyika kwa ajili ya mazishi hayo kufanyika leo. Ngosha aliyezaliwa mwaka 1965, ameacha mjane na watoto kumi

1 comment:

  1. Twamuombea mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi na pole kwa wafiwa wote, kwani yote ni mapenzi yake Rabana

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages