Breaking News

Your Ad Spot

Jan 13, 2011

YANGA YALALA KWA SIMBA ZANZIBAR; YATUNGULIWA 2-0






TIMU ya Yanga imeshindwa kufurukuta kwa Simba, baada ya kutandikwa mabao 2-0, katika mechi ya fainali ya Kombe la Mapinduzi, kwenye Uwanja wa Aaman mjini Zanzibar.
Ni bao lililofungwa na Shija Mkina lililoiwezesha Simba kuibuka na ubingwa. Kutokana na matokeo hayo, Simba imeanza mwaka kwa kuwafunga watani wao na kulipiza kisasi cha kufungwa na timu hiyo zilipokutana katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara mwaka jana mjini Zanzibar.

Yanga ndiyo iliyoanza mchezo kwa kasi huku ikitandaza kandanda safi na wachezaji wake kucheza kwa kuelewana kwa kugongeana pasi fupifupi ambazo wachezaji wa Simba walishindwa kuzidhibiti takribani dakika tano za mwanzo za mchezo huo.,


Dakika ya tisa, Yanga ilipata nafasi ya wazi kwa Idd Mbaga kumtoka beki wa Simba Jerry Santo lakini akaachia shuti lililoishia mikononi wa kipa wa Simba Ally Mustapha.

Simba ilijibu shambulizi hilo dakika ya 12 kupitia kwa Patrick Ochan aliyepiga shuti ambalo kipa wa Yanga Yaw Berko alitema kabla ya mabeki kuondosha mpira huo katika eneo la hatari.

Dakika moja baadae Simba iligfanya shambulizi jingine kupitia kwa Hiraly Echesa aliyepiga shuti kali baada ya kupata nafasi ya wazi lakini mabeki wa Yanga walizuia hatari hiyo na kuokoa mpira golini kwao.

Simba iliendelea kufanya mashambulizi makali langoni mwa wapinzani wao huku ikitafuta mabao ya kufunga na dakika ya 20 Mussa Hassan 'Mgosi' alipata nafasi baada ya kubaki na kipa lakini shuti hafifu alilopiga lilijaa mikononi mwa Berko.

Dakika ya 33 Mussa Hassan 'Mgosi' aliipatia Simba bao la kwanza baada ya kupokea pasi safi iliyopigwa kutoka wingi ya kulia na kuachia shuti kali lililomshinda kipa Yaw Berko wa Yanga na kujaa moja kwa moja wavuni.


Kipindi cha kwanza kilimalizika kw Simba kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa nbao 1-0, na kipindi cha pili kilipoanza Simba ilianza mchezo kwa kasi huku ikitafuta mabao mengine lakini mabeki wa Yanga walikaa imara na kuzuia hatari zilizojitokeza katika lango lao.


Hata hivyo mabeki wa Yanga hawakufua dafu kwa watoto wa Msimbazi ambao kila dakika zilivyozidi kuyoyoma ndivyo walivyozidisha mashambulizi huku wachezaji wa Yanga wakionekana kupoteana.

Yanga nao walifanya mashambulizi ya kushitukiza langoni mwa Simba kila walipopata nafasi lakini umaliziaji mbovu na shuti hafifu alizopigiwa kipa Ally Mustapha ziliifanya timu hiyo kushindwa kupata walau bao moja.

Laiti kama Simba ingetumia vyema nafasi nyingine ilizopata dakika ya 49, 52 na 66 kupitia kwa Jerry Santo, Mgosi na Echesa ingeweza kupata mabao mengi zaidi lakini umaliziaji uliifanya timu hiyo kushindwa kufunga mabao mengine.

Kutokana na ushindi huo Simba wamepata kombe lenye thamani ya sh. milioni 3 na fedha taslim sh. milioni 5.

Kwa mara ya kwanza Simba  iliifunga Yanga mjini Zanzibar kwa ambapo mwaka 1992, katika fainali ya kombe la Kagame ilishinda kwa mikwaju ya penalti 6-5.

Vikosi: Simba:- Ally Mustapha, Haruna Shamte, Meshack Abel, Jerry Santo, Abdulrahim Humoud, Mohamed Banka, Hirally Echesa, Mussa Hassan 'Mgosi' Patrick Ochan na Nico Nyagawa.


Yanga:Yaw Berko, SalumNtelela, Abuu Ubwa, Isack Boakye, Job Ibrahim, Ernest Boakye, Godfrey Bonny, Juma Seif, Razack Halfan/Kigi Makasi, Idd Mbaga na Davis Mwape.

2 comments:

  1. gday bashir-nkoromo.blogspot.com owner found your site via yahoo but it was hard to find and I see you could have more visitors because there are not so many comments yet. I have discovered website which offer to dramatically increase traffic to your site http://xrumerservice.org they claim they managed to get close to 1000 visitors/day using their services you could also get lot more targeted traffic from search engines as you have now. I used their services and got significantly more visitors to my site. Hope this helps :) They offer most cost effective backlinks service Take care. Jason

    ReplyDelete
  2. WMID 161179576531 КИДАЛА НА ОБМЕНАХ И ИГРОВЫХ ВАЛЮТАХ
    ICQ: 625904048 WMID: 161179576531 - обменник
    Обмен WMR|WMZ|WMU <=> ЯД
    Номер ICQ: 625904048
    Номер ICQ: 643511912
    E-mail: legitlex@mail.ru
    E-mail: obmanoff.net@mail.ru
    E-mail: vishneckiir@mail.ru
    Номер телефона: 380968106922
    Адрес: Донецк, улица Артема, дом 147г
    Интернет сайт: www.obmanoff.net
    Интернет сайт: www.legitlex.com
    Интернет сайт: www.zadrotoff.net
    WMID: 161179576531
    WMID: 129742512414
    Счет WMR: R112397336005
    Счет Яндекс деньги: 410011068058555
    Этот человек является незаконным владельцем портала www.obmanoff.net + занимается обманом и мошенничеством через сайты www.legitlex.com, www.zadrotoff.net
    Фрилансер который делал ему сайт www.obmanoff.net не получил за работу ни копейки и помимо этого был добавлен в базу кидал www.obmanoff.net как недобросовестный исполнитель, при этом мы видим, что сайт вполне рабочей и неплохо функционирует, но еще интересней то, что в эту же базу попадают все, кто помогает Роману в работе над сайтом и естественно, за свою работу они получают только головные боли и неприятности.
    http://free-blacklist.ru/blacklist/212/
    http://free-blacklist.ru/blacklist/224/
    Под видом продажи игровой валюты профессионально занимается кардингом, отмывая через продажу адену.
    КРАЙНЕ НЕ СОВЕТУЮ ИМЕТЬ ДЕЛО С ЭТИМ ЧЕЛОВЕКОМ. ПОКУПАТЬ - ПРОДАВАТЬ - МЕНЯТЬ! (совсем недавно этот "уникум" занялся "обменом" валюты)! БУДЬТЕ БДИТЕЛЬНЫ!
    Он уже кинул 4 человека на обмене.
    Не советую иметь дело с этим человеком.

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages