Breaking News

Your Ad Spot

Feb 22, 2011

MABOMU GONGOLAMBOTO: KAMATI YA BUNGE MAMBO YA NJE NA SPIKA WATEMBELEA MAENEO YA TUKIO; MISAADA YAZIDI KUMIMINIKA, YANGA UPANDE WA TIMU ZA SOKA, TWANGA UPANDE WA BENDI ZA MUZIKI

SPIKA wa Bunge Anna Makinda akimkabidhi Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, hundi ya Sh. milioni 37.80,  leo, kweye kituo cha uratibu na kupokea misaada kwa ajili ya waathirika wa mabomu ya Gongo la Mboto, kilichopo, Ofisi ya Mtendaji Kata ya Ukonga.Fedha hizo zimetolewa na wabunge kwa kusaidia wananchi walioathirika ma mabomu hayo. Kulia ni Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Mecky Sadiki.
MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Edward Lowassa, akikaribishwa na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange, yeye na kamati hiyo walipotembelea leo, kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzaniani, Gongo la Mboto, Dar es Salaam, kufahamu mazingira na hasara ya milipuko ya mabomu iliyotokea katika ghala la silaha la JWTZ katika kambi hiyo, Jumatano iliyopita. 
MWENYEKITI wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Dar es Salaam, ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa mkoa huo, Saidi Mecky Sadiki (kushoto), akitoa taarifa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, kuhusu  mwenendo na hatua zilizochukuliwa na serikali ya mkoa huo, dhidi ya maafa ya milipuko ya mabomu ya Gongo la Mboto,Waziri Nahodha alipotembelea kituo cha  tathmini na kupokea misaada kwa waathirika wa mabomu hayo, kilichopo Ofisi ya Mtendaji Kata ya Ukonga, leo. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inpekta Jenerali, Saidi Mwema

Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha akiwaachia maelekezo , Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inpekta Jenerali, Saidi Mwema na Kova


Mwenyekiti wa CUF, Prof, Ibrahim Lipumba akibeba kiroba cha unga uliotolewa msaada na chama chake kwa ahili ya waathiriwa wa mambomu 
Wachezaji wa Yanaga wakimkabidi msaada wao Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Anayekabidhi ni Fred Mbuna.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema,  Victor Kimesela akikabidhi msaada wa shuka 166 kweneye kituo cha Ofisi ya Mtendaji Ukonga.
Wafanyakazi wa TiGo wakikabidhi msaada wao kituo cha kupokela misaada cha Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Ukonga.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages