Breaking News

Your Ad Spot

Feb 5, 2011

SUPER D KUANDAA FILAMU

BONDIA wa Zamani na Kocha wa Ngumi wa Klabu ya ngumi ya Ashanti, Rajabu Mhamila 'Super D' yupo mbioni kutoa Video itwayo 'Super D Boxing Coach' inayozungumzia maisha yake ya mchezo huo.

        Akizungumza Dar es Salaam jana, Super D alisema video hiyo itakuwa sokoni muda wowote kuanzia sasa ikizungumzia maisha yake tangu alipoanza kucheza mchezo huo mwaka 1984 hadi sasa.
  Aliisema Video hiyo itaonesha mapambano mbalimbali aliyocheza na dhidi ya mabondia Mbwana Matumla, Rashidi Ali na Ajibu Salumu.
  Alisema lengo la kuandaa video ni kutaka kutimiza malengo yake ya kuendeleza mchezo wa ngumi kwa kuwapatia vijana nafasi ya kujifunza kupitia kwake.
      Alisema kutokana na nchi ya Tanzania kuwana vipaji vingi atashindwa kuwafikia kila mmoja wao na badala yake amewapa fursa ya kujifunza kwa kuangalia video.
Alisema Video katika kuhaikisha Video hiyo inafanya vizuri sokoni ameongezea vionjo vingine kutoka kwa mabondia maarufu duniani kama Mike Tyson, Michael Mo, Junior Myweather, Mohamed Ally, Man Paqyao na Joe Fleizer.

1 comment:

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages