Breaking News

Your Ad Spot

Mar 31, 2011

MBUNGE WA MCHINGA AIPIGA TAFU UHURU QUEENS

Mbunge wa Jimbo la Mchinga Mheshimiwa Said Mtanda , jana amefanya mambo yazidi kuwa mazuri kwa timu ya netiboli ya  Uhuru Queens kwa kuipatia sh. 100,000 taslim, kwa ajili ya kusaidia matumizi ya wachezaji wa timu hiyo inayoshiriki michuano ya Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF). Pichani, mbunge huyo akimkabidhi fedha hizo, kwa  mchezaji wa timu ya Uhuru Queens Salome Mwasamale, katika chumba cha habari cha Uhuru Publications Ltd, mtaa wa Lumumba mjini Dar es Salaam. Michuano hiyo inaendelea katika viwanja vya TTC Chang'ombe  ambapo Uhuru Queens inaongoza katika kundi C la mashindano hayo ikiwa na pointi sita hadi sasa. Wanaoshuhudia makabidhiano hayo kutoka kushoto ni Mdau wa timu hiyo, Laurencia Masota, Meneja wa timu Jane Mihanji na Mhariri wa gazeti la Burudani Rashid Zahoro.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages