Breaking News

Your Ad Spot

Mar 24, 2011

SERENGETI BEER YAIPA STARS MILIONI 100 KWA AJILI YA MECHI YAKE NA AFRIKA YA KATI: VIJANA NAO WAONDOKA LEO KWENDA CAMEROUN

KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL), imetoa sh. milioni 100, kusaidia timu ya Taifa, Taifa Stars katika mechi ya timu hiyo na Afrika ya Kati, kesho kwenye Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam. Pichani, Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo, akimkabidhi mfano wa hundi ya fedha hizo Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Nchini (TFF), Angetile Oseah, katika Ofisi za TFF mjini Dar es Salaam, leo. Mbele ni Kocha mkuu wa Stars Jean Poelsen na wachezaji wa timu hiyo, Nahodha, Shadrach Nsajigwa na Mshambuliaji, Athumani Machupa.

WACHEZAJI wa timu ya Taifa ya Vijana, wakiwa katika basi katika Ofisi za Shirikisho la soka Tanzania (TFF), kwa ajili ya kwenda Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam, jana, tayari kwa safari ya kwenda  Cameroun, kwenye mechi yao na timu ya vijana ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages