Breaking News

Your Ad Spot

May 4, 2011

MTAYARISHAJI WA BLOGU HII APATA TUZO YA MPIGAPICHA BORA TUZO ZA EJAT 2011


MENEJA Mipango wa Mfuko wa Ruzuku kwa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF)
Ernest Sungura (kushoto) akimkabidhi tuzo ya mpigapicha bora wa picha za habari,
Mpigapicha Mwandamizi wa Kampuni ya Uhuru Publicatiosn Ltd, Bashir Nkoromo,
baada ya kushinda tuzo hiyo, katika hafla ya utoaji Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa
Habari (EJAT), jana, katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam. 
 Mtayarishaji Mkuu wa Blogu hii, ambaye ni mpigapicha wa magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, Bashir Nkoromo, ameng'ara katika Tuzo ya Umahiri ya Uandishi wa Habari (EJAT) kwa mwaka 2010.
Nkoromo aliibuka mshindi wa picha bora dhidi ya Mpigapicha wa magazeti ya Daily News na Habari Leo, Robert Okanda, na kukabidhiwa tuzo, cheti na zawadi ya kamera.
Katika hafla hiyo iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, Mhariri wa Habari wa Uhuru FM, Pius Ntiga, alipata Tuzo ya Elimu akimshinda Adeladius Makwega wa TBC Taifa.
Akishukuru baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Nkoromo alisema kwamba ushindi wake haumaanishi kuwa yeye ni bora zaidi ya wapigapicha wengine katika vyombo vya habari, bali picha aliyoipiga ambayo imempatia ushindi ndiyo ilikuwa bora.

Wadau mbalimbali wa sekta ya habari walihudhuria hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa, Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samatta.

Tuzo nyingine kadhaa zilikwenda kwa waandishi wa habari, watangazaji wa redio, televisheni na wachoraji wa katuni wa vyombo mbalimbali vya habari.

Akizungumza kweye hafla hiyo, Katibu Mtendaji wa Baraza la habari Tanzania (MCT), Kajubi Mkajanja,alisema utozji tuzo hizo umefikiwa baada ya kupata wateule 76, kupitia na kuchuja kazi 437 zilizowasilishwa na waandishi mbalimbali wa habari katika makundi 16 ya tuzo zinazoshindaniwa.
Mtia Chachandu za habari Mkuu wa Blogu hii, Bashir Nkoromo akiwa na tuzo na zawadi ya Kamera aliyotuzwa kwa kuibuka mpigapicha bora wa tuzo za EJAT 
Tuzo ya cheti

Fatuma Said Abdallah mwenye umri wa zaidi ya miaka 70, akisaidiwa na kijana, Saidi Haji baada ya kupigakura katika kituo cha Fuoni, wilaya ya mjini Magharibi, wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka jana. Picha hii ndiyo iliyoshinda tuzo hiyo

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages