Breaking News

Your Ad Spot

Jul 21, 2011

MWILI WA NAIBU MKURUGENZI WA MAELEZO WAAGWA DAR, KUZIKWA KESHO MTO WA MBU ARUSHA

Mwili wa Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Sozzy Mahmoud aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana umesafirishwa leo kwenda Mto wa Mbu Arusha kwa ajili ya Mazishi. Msafara wa kuuplele Mto wa Mbu mwili wa Sozzy ambaye alikuwa mke wa Mkurugenzi wa Uhuru FM,
Mikidadi Mahmoud ulianzia nyumbani kwao, Karakata, Kipawa Dar es Salaam.
Waombolezaji wakishusha jeneza kutoka kwenye gari. 
Marehemu Sozzy 
Waombolezaji wakiangua vilio baada ya mwili wa marehemu Sozzy kufikishwa nyumbani. 
Waandishi wa habari waandamizi waliokuwa karibu na Sozzy wakiwa katika majonzi mazito wakati wa kuagwa mwili wa marehemu. 
Baadhi ya waombolezaji wakisoma kisomo maalum 
Mhariri Mtendaji wa Uhuru Publications Ltd, Josiah Mufungo na maofisa wa kampuni hiyo wakiwa kwenye msiba. 
Waombolezaji kadhaa wa kadhaa wakiwepo msibani 
Waombolezaji wengi walikuwa kutoka Idara ya Habari (MAELEZO), Uhuru FM na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, ukitazama kwa makini picha hii utawaona wanaotoka ofisi hizo. 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi akitia saini kitabu cha maombolezo ya Souzzy. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Seth Kamuhanda. 
Waziri Nchimbi (kushoto) akimpa pole mume wa marehemu. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama na watatu ni Mzee Kingunge Ngombale-Mwiru 
Mahmoud (kulia) akimweleza Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye jinsi kifo kilivyomfika marehemu Sozzy 
"Marehemu alikuwa na mchango mkubwa katika sekta ya habari " pengine ndivyo Nape na Waziri Nchimbi walivyokuwa wakisema hapa, wakati wa kuangwa marehemu Sozzy 
"Sana Waziri,  huyu alikuwa kamanda katika wapiganaji kwenye eneo moja wapo la wizara yako," pengine hapa napo Nape alisema hivyo kwa Waziri Nchimbi.
Mahhoud akimshukuru Waziri Nchimbi baada ya kutoa salamu za  rambirambi. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama na Kushoto ni Nape 
Wadau kibao walihudhuria kuagwa kwa Sozzy. Kulia ni aliyekuwa Mkurugezi wa TBC, Datsun Tido Mhando 
Wafanyakazi katika Ofisi Ndogo ya Makau Makuu ya CCM 
Wadau wengine kama wanavyoonekana pichani.  
Jeneza lenye mwili wa Sozzy likitolewa ndani tayari kwa safari 

Likawekwa nje na kuswaliwa na waombolezaji 
Katibu Mkuu wa CCM ni miongoni mwa waliotoa salamu za rambirambi. 
Waziri Nchimbi alihitimisha kwa kutoa salamu za rambi rambi kabla ya safari ya kuupeleke mwili Sozzy kuanza.
Mzee Madanga Shaaban Madanga (aliyeshika tama) ni miongoni mwa waombolezaji walifika msibani hapo. 
Basi likiondoka nyumbani kwa Mzee Mikidadi Mahmoud kwa safari ya Mto wa Mbu, Arusha, likiwa na mwili wa marehemu Sozzy.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages