Breaking News

Your Ad Spot

Jul 27, 2011

ZIARA YA RAIS KIKWETE MTWARA

Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimtwika ndoo ya maji bi.Zainab Yusuf Lidandi wakati Rais alipokagua na kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Nyundo wilaya ya Mtwara vijijini jana jioni.Rais Kikwete yupo mkoani Mtwara kwa ziara ya kikazi kukaguana kuzindua shughuli mbalimbali za maendeleo.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Nyundo Mtwara vijijini jana jioni muda mfupi baada ya kukagua na kuzindua mradi wa maji kijijini hapo.Mradi huo unafadhiliwa na shirika la AMREF.
Mtafiti wa zao la Korosho katika kituo cha utafiti wa Mazao na mafunzo cha Naliendele Mtwara, Dr.Peter Masawe akimpa maelezo Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wakati Rais kikwete alipokitembelea kituo hicho jana mchana kukagua maendeleo ya tafiti za mazao mbalimbali.Baadaye Rais kikwete alikutana na uongozi wa kituo hicho na kujadili namna ya kuboresha shughuli za kituo hicho muhimu.
Mtafiti wa Muhogo na jamii ya viazi Dr.Geofrey Mkamilo(kulia) akimwonesha Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete muhogo ulozalishwa kwa kutumia mbegu bora ya Naliendele wakati Rais alipotembelea kituo cha Mafunzo na utafiti wa mazao huko Naliendele,mkoani Mtwara jana mchana. 4---7048—Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Nyundo Mtwara vijijini jana jioni muda mfupi baada ya kukagua na kuzindua mradi wa maji kijijini hapo.Mradi huo unafadhiliwa na shirika la AMREF (PICHA ZOTE NA FREDDY MARO)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages