Breaking News

Your Ad Spot

Aug 30, 2011

WATUHUMIWA WA UJAMBAZI WAUAWA DODOMA;WANANCHI WAPANGA FOLENI KUONA MAITI

 Kamanada wa Polisi wa mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen akionyesha  gamba lisilopenywa risasi lililonusuru maisha ya polisi wake katika mapambanao na majambazi katika pori la Goma, barabara ya manyoni-Singida nje kidogo ya mji wa Dodoma, wiki iliyopita. katika tukio hilo watuhumiwa wanne wa ujambazi waliuawa na polisi
 Wananchi wakijaribu kunyanyua ili kujua uzito wa gamba lisilopenya risasi ambalo lilinurusu maisha ya polisi yaliokuwa wakipambana na majambazi wa kurushiana risasi katika msitu wa Goama, nje kidogo ya mji wa Dodoma wiki iliyopita.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen  akionyesha bunduki iliyotengenezwa kienyeji inayosadikiwa walikamatwa nayo watuhumiwa wanne  wa ujambazi waliouawa mjini humo wiki iliyopita katika majibishano ya risasi na polisi nje kidogo ya mji wa Dodoma.
wananchi wakipanga foleni kuingia chumba cha maiti cha hospitali ya mjini Dodoma kutambua maiti za watu wanne waliouawa na polisi katika majibishano ya risasi wakituhumiwa kwa ujambazi wa kuteka mabasi katika barabara kuu ya Manyoni-Singida. 
Wananchi watazama maiti za watuhumiwa wa ujambazi iliyowekwa katika chumba cha maiti hospitali ya mkoa wa Dodoma 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Zelothe Stephen na Mkuu wa mkoa wa  Dodoma Dk James Nsekela na Mganga Mkuu wa hospitali ya Dodoma, Dk. Godfrey Mtei wakitoka katika chumba cha maiti kwenye hospitali  hiyo (Picha zote na Emmanuel Ndege aliyekuwa Dodoma)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages