Breaking News

Your Ad Spot

Dec 29, 2011

MAHAKAMA MISRI YAZUIA KUWAPIMA BIKIRA AMBAO HAWAJAOLEWA

Mahakama katika mji wa Cairo nchini Misri imepinga kitendo kilichofanywa na Baraza la Kijeshi la Misri cha kuwapima bikra wasichana saba waliokamatwa kwenye maandamano, ikisema ni kinyume cha sheria na inabidi wasichana hao walipwe fidia.

Jaji wa mahakama hiyo,  Aly Fekry ametoa uamuzi huo katika kesi iliyofunguliwa na msichana Samira Ibrahim (25), ambaye alisema yeye na wenzake  sita waliteswa na kudhalilishwa na wanajeshi hao baada ya kukamatwa kwenye Uwanja wa Tahrir wakati wa maandamano yaliyofanyika Machi 9, mwaka huu.

Semira alikuwa miongoni mwa waandamanaji 200 waliokamatwa siku hiyo 20 kati yao wakiwa ni wanawake.

Alisema siku iliyofuata  wanawake hao walitenganishwa makundi mawili kwa kuwaweka walioolewa kundi lao na ambao bado ambao walikuwa saba waliwekwa kundi la pili na kuamriwa wapimwe bikira na madaktari wanaume.

Walisalimika baada ya kukutwa na bikira zao, lakini kama wangekutwa hawana wangefunguliwa mashikata ya kufanya umalaya. 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages