Breaking News

Your Ad Spot

Dec 20, 2011

MREMBO WA VENEZUELA AFARIKI DUNIA

Eva Ekvall
CARACAS, Venezuela
Miss Venezuela wa zamani, Eva Ekvall, amefariki dunia kwa ugonjwa wa saratani ya matiti, akiwa na umri wa miaka 28.

Kwa mujibu wa mtandao wa Yahoo, familia yake imesema Ekvall amefariki Jumamosi katika hospitali ya Houston.

Ekvall alitwaa taji la urembo wa  Venezuela  mwaka 2000 akiwa na umri wa miaka 17 na mwaka uliofuata alitwaa nafasi ya tatu katika shindano la Miss Universe lililofanyika mjini Puerto Rico. Aliendelea kufanya kazi ya uanamitindo, mwigizaji wa filamu na mtangazaji wa habari katika televisheni.

Mrembo huyo amewahi kuandika kitabu "Fuera de Foco" ("Out of Focus"), kuhusu mapambano ya saratasni ambacho kilitumia picha za mpigapicha wa Venezuela Roberto Mata.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages