Breaking News

Your Ad Spot

Dec 20, 2011

MAHAFALI YA MZUMBE KAMPASI YA DAR

Mahafali hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki yalikuwa ya aina yake, hasa kwa wahitimu kumeremeta katika majoho kama hawa ndugu waliojipatia shahada ya pili ya sayansi katika Menejimenti ya Ununuzi.  Kama unayafahamu majina yao nitajie kweneye  maoni hapo dauni.
 Hawa wao walipata  "Master Of Business Asdministration (MBA) Corporate Management.
 Nawa pia wanaopiga pozi usawa wangu wa kamera wamepata shahada hiyo hiyo ya MBA....
 Hawa bila shaka ungependa kujua majina yao kwa jinsi wanavyoonekana wenye furaha. Tafadhali anayewafahamu atuwekee hayo majina yao kwenye maoni chini ya ukurasa huu.
 Maandalizi ya kila aina yalihitajikamuda mfupi kabla ya wahitimu kutunukiwa shahada zao, Huyu ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwekwa sawa kofia yake na Mama yake mzazi mbaye kwa heshima nitamwita 'Mama Nape' basi. Kulia anayeshuhudia ni  Mkuu wa Kitengo wa Mahusiano na Umma katika Idara ya Itikadi na Uenezi Makao Makuu ya Chama, Comrade Chongolo.
 Kutokana na kuwa siku ya kipelee wahitimu karibu wote walisindikizwa na familia zao, huyu ni Ofisa Makao Makuu ya CCM pale Lumumba, Ndugu Mpelemba akipozi picha pamoja na wanafamilia yake.
Dada Emiliana wa Uhuru Publications Ltd, Wachapishaji wa magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani akimpongeza ndugu wake aliyepiga nondozzz hapo hapo Mzumbe. Bila Shaka Dada Emmy atatuwekea jina la huyu ndugu yake kwenye maoni chini ya ukurasa huu.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages