Breaking News

Your Ad Spot

Feb 3, 2012

TUJIPANGE KUWASAIDIA VIJANA NA MASKINI-MIGIRO


Na Mwandishi Maalum, New York
Imeelezwa kwamba linapokuja suala la ukofesu wa ajira,  vijana ndio wanaoathirika zaidi  ikilinganishwa na watu wazima.
      Akifungua mkutano wa 50 wa Tume ya Maendeleo ya Jamii ya Umoja wa Mataifa,  Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Asha-Rose Migiro (pichani kushoto) amewaeleza wajumbe wa mkutano huo kwamba,  linapokuja  tatizo la ajira,  vijana huadhirika mara tatu zaidi ya watu wazima.
      “ Takwimu za  Shirika la Kazi Duniani (ILO)zinaonyesha kwamba  mtu mmoja  katika kila watu watatu,duniani ama  hana ajira au anaishi katika umaksini. Hii ni sawa na zaidi ya watu bilioni moja”. Anasema Naibu Katibu Mkuu na kuongeza. 
     “Lakini  vijana hasa ndio walioathirika zaidi. Ukosefu wa ajira kwao ni mara tatu zaidi ya watu wazima na kwa mwaka jana tu vijana milioni 75 walikuwa hawana ajira” anasema Migiro.
     Tume ya Maendeleo ya Jamii  ya Umoja wa Mataifa ambayo imeanza mkutano wake siku ya jumatano itakutana kwa siku kumi hapa  Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
     Pamoja na kupokea taarifa mbalimbali, wajumbe wa Tume watajielekeza zaidi katika kujadiliana na kuweka mikakati na mipango madhubuti ya kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana, upunguzaji wa umaskini, mdororo wa uchumi na  athari zake kwa maendeleo ya watu na hasa watu maskini na mabadiliko ya tabia nchi.
    “Tunaishi katika  nyakati za mashaka, mdororo wa uchumi unaendelea kuchukua mkondo wake. Na matokeo yake ni kuendelea kujengeka kwa chuki miongozi  mwa jamii”. anabainisha Naibu Katibu Mkuu.
        Kama hiyo haitoshi, Migiro anasema , pengo  kati ya matajri na maskini  linazidi kuongezeka na , umaskini unaongeza shinikizo katika familia nyingi.
    “ katika  familia ambayo kuna uhaba mkubwa wa chakula na  fedha ni chache, ni wazi kwamba hali ya uvumilivu hutoweka na mifarakano hujitokeza.Lakini pia  matukio ya watu kujiua  huongezeka,  matumiziya dawa za kulevya yamekithiri huku vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wanawake na  watoto  navyo vikiongezeka”.
   Akasema  vijana ambao ndio tegemeo kubwa hivi sasa wanashindwa kujua nini hatima yao, hawana matumaini tena na wanazidi kukata tamaa ya maisha.
        Akaongeza kwamba, maskini wanataka kujinasua kutoka katika dimbwi la umaskini, ni kwa sababu hiyo  Umoja wa Mataifa kupitia Tume hiyo inatakiwa kwa kweli,  kuwa na  sera za kuilinda jamii. Kwa   maana ya  kuwa na uhakika wa kuwa  na chakula, elimu na huduma za msingi hasa kwa maskini.
   “Maskini  wanataka kujisaidia wao wenyewe na familia zao, tunatakiwa kuwajengea fursa nzuri za ajira.
anasisitiza.
     Kwa upande wake Rais wa Baraza la  Uchumi na Jamii Maendeleo la Umoja wa Mataifa, (ECOSOC) Balozi  Milos Koterec, akizungumzia kuhusu ukosefu wa ajira kwa vijana.
     Yeye amesema   katika mkutano huo pamoja na mambo mengine, Tume  ya Maendeleo ya Jamii itatoa kipaumbele maalumu kwa vijana na hususani changamoto ya ukosefu wa ajira.
   Akasema  katika nchi zilizoendelea  katika kila vijana wanne mmoja hana ajira. Ili hali   idadi kubwa ya vijana katika nchi zinazoendelea wanajaribu kubangaiza kwa  kujiajiri katika sekta zisizo rasmi.
    “ Dunia inashuhudia mgogoro mkubwa wa ukosefu wa ajira kwa vijana, ukosefu unaochangia katika uvunjifu wa amani na  tishio la usalama  katika jamii”. Akasisitiza Balozi Koterec..
   Aliongeza kwamba ukosefu huo wa ajira kwa vijana, kunawasukuma  kujiingiza katika vitendo vya kudai demokrasia, fursa sawa na  kazi zenye tija.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages