Breaking News

Your Ad Spot

Mar 16, 2012

MAZISHI YA ALIYEKUWA MWAKILISHI WA BUBU LEO

 Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein pamoja na viongozi wengine wa kitaifa wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakishiriki kumuombea dua aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu CCM Marehemu Salum Amour Mtondoo aliyefariki  kutokana na ugonjwa wa shindikizo la damu huko katika hospitali ya
Mnazi Mmoja Zanzibar
 Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai akitoa hotuba kwa niaba ya Chama cha Mapinduzi CCM kuhusu utendaji kazi wa Marehemu katika chama hicho enzi za uhai wake
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein watatu kulia akiitikia dua iliyokuwa ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Skh. Omar Kaabil,kuliani kwa Rais ni Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Shariff Hamad pamoja na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi,kushotoni kwa Rais ni
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd. (Picha zote na Yussuf Simai Maelezo Zanzibar)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages