Breaking News

Your Ad Spot

Mar 16, 2012

KAMPENI ARUMERU: SIOI ACHANGAMKIWA NA WANANCHI WALIOFURIKA MKUTANONI KATA YA MAKIBA

 Mgombea ubunge wa CCM jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari akibebwa na wananchi kumpeleka jukwaani kuomba kura kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Uwanja wa mpira wa kamji kalikochangamka sana ka Kata ya Makiba jimboni humo jana.
 Sioi akiomba kura kwa wananchi katika mkutano huo. Kushoto ni Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na kulia ni Mratibu wa kampeni za CCM kitaifa, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba.
 Mama wa Kizanzibari, Katibu wa NEC Oganaizesheni CCM, Asha Abdallah Juma aka Mshua akisalimia wananchi katika mkutano huo
KIBAJAJI NA  STAILI YA JOGOO! "Chadema sera zao za uongo kama jogoo...akiwa na jike anadanganya nitakununulia kanzu ndeeeefu hadi miguuni, lakini jogoo mwenyewe akiinama hana hata nguo ya ndani", Mbunge wa Mtera Joseph Lusinde aka Kibajaji akisema hivyo huku akionyesha kwa vitendo kwenye mkutano huo wa Makiba.
  Jenerali Mstaafu, Sarakikya akimuombea kura Sioi kwenye mkutano huo. Alipanda jukwaani kwa niaba ya wazee wa Kata ya Makiba.
 Msanii maarufu Hafsa Kazinja akifanya manjonjo yake kuwaburudisha wanancji wakati wa mkutano huo
 "CCM DOLE TUUUU" ni maneno ya shabiki huyu wa CCM aliyokuwa akiyatoa mara kwa mara anapokunwa na hotuba za viongozi kwenye mkutano huo Kata ya Makiba
 Sehemu ya maelfu ya wananchi waliofurika mkutanoni Kata ya Makiba
Mwigulu akihutubia kadamnasi

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages