Breaking News

Your Ad Spot

Mar 9, 2012

MKUTANO WA JK NA WAZEE ULIOKUWA UFANYIKE LEO SASA NI KSHO

Rais Jakaya Kikwete

Mkutano wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam uliopangwa kufanyika leo, Ijumaa, Machi 9, 2012, umeahirishwa hadi kesho, Jumamosi, Machi 10, 2012.

Mkutano huo umeahirishwa ili kutoa nafasi kwa Mheshimiwa Rais kufanya mashauriano zaidi na wadau mbali mbali kuhusu suala ambalo Mheshimiwa Rais atalizungumzia kwenye mkutano huo.

Kama ulivyokuwa mkutano ulioahirishwa leo, mkutano wa kesho utafanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee kuanzia saa tano asubuhi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages