Breaking News

Your Ad Spot

Mar 19, 2012

WAZIRI TEREZYA HOVIZA TEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa  Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayehusika na Mazingira Mhe. Terezya Hoviza  (Mb)akimsikiliza Kaimu Balozi   Bw.Justin Seruhere, wakati Waziri huyo na ujumbe wake alipoutembeleza Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  katika Umoja wa Mataifa,  ulipo jijini New York, Marekani. Mhe. Waziri Hoviza alikuwa hapa kuhudhuria mkutano wa siku mbili wa kilele ulioandalliwa na   Taasisi isiyo Kiserikali   ya World Society of Protection of Animals ya Switzland. Mkutano huo ambao uliwashirikisha wajumbe kutoka nchi mbalimbali duniani  ajenda kuu  ilikuwa  ni  Chakula, Lishe na  Lilimo Endelevu. Waziri  Terezya  Hoviza alikuwa mmoja wa wajumbe waliozungumza katika mkutano huo na pia aliongoza   moja ya mijadala ya  mkutano huo.
 Akatumia  fursa hiyo kuelezea uzoefu wa Tanzania katika uboreshaji na uendelezaji wa kilimo endelevu na chenye tija,  uhifadhi wa chakula na suala zima la lishe. Tanzania ni kati ya nchi chache  katika bara la Afrika ambazo zinazalisha chakula cha kutosha  na   ziada kuunzwa  katika nchi za jirani. Mwishoni mwa mkutano huo wajumbe walitoka na azimio ambalo litawasilishwa kwa  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki  Moon, ili  mapendekezo yaliyomo katika azimio  hilo   yaweze kuingizwa kwenye Tamko  la Pamoja la Mkutano wa Kimataifa wa  Maendeleo Endelevu maarufu kama RIO +20. Mkutano huo utafanyika mwezi June mwaka huu huko Rio de Janeiro, Brazil.


Kutoka kushoto ni Katibu wa Waziri, Bw. Joseph Qamara, Mhe. Waziri Terezya Hoviza( Mb)  Kaimu Balozi,Bw. Justin Seruhere na Bw. Julius Ningu Mkurugenzi wa Mazingira

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages