Breaking News

Your Ad Spot

Apr 28, 2012

WANANCHI WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI MONDULI


Na Rose Jackson,Arusha
WANANCHI zaidi kutoka   kata ya Lepurko Wilayani Monduli Mkoani Arusha  wanaokabiliwa na ukosefu wa maji hivi sasa watanufaika na mradi wa maji ya bwawa la kisasa linalojengwa katika kijiji cha Nanja  Wilayani humo.
     Bwawa hilo pia litasadia mifugo zaidi ya   elfu ishirini kupata maji na kupunguza kuenea kwa magonjwa ya mifugo  katika maeneo hayo.
     Kwa mujibu wa wananchi hao walikuwa wakitembea mwendo wa kilomita zaidi ya kilomita zaidi ya kumi na tano  kutafuta bidhaa hiyo adimu katika eneo hilo la wafugaji wa kimasai.
     Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa kijiji cha Nanja  eneo linakojengwa  bwawa hilo Tingide Shamburi  alisema kuwa  bwawa hilo linajengwa na kampuni  inayokarabati  barababara ya Arusha Minjingu ya Sogea Satom ya nchini Ufaransa.
    Alisema kuwa tatizo la kufuata  maji katika maeneo ya mbali pia limekuwa likichangia kuenea kwa magonjwa ya mifugo na kusababisha wafugaji kupoteza mifugo yao .
    Tingide aliongeza kuwa  wanawake wamekuwa wakijeruhiwa na wanyama nyakati za usiku wakati wakifuata maji katika vijiji vya jirani katika eneo hilo lililopo karibu na hifadhi taifa. 
    Aidha aliwashukuru wahisani hao kwa kuamua kuwasaidia kuondokana na tatizo hilo aambalo limekuwepo katika maeneo yao kwa miaka mingi.
    Alisema kuwa kwa mujibu wa wataalamu bwawa hilo litadumu kwa muda mrefu kutokana na kuwekewa kitambaa maalumu katika sakafu yake  ili kutoruhusu maji kupotelea ardhini.
    Kwa upande wake afisa uhusiano wa kampuni  SOGEA SATOM ya nchini Ufaransa   Jamal  Nassoro Addi alisema kuwa  bwawa hilo litagharimu shilingi miloni mia moja za kitanzania  na litakamilika katika kipindi cha wiki mbili zijazo.
    Addi aliongeza kuwa  kampuni yake iliamua kutoa msaada kwa wananchi  kama sehemu ya kuonyesha utu.
    “Kimsingi sisi hatukuwa na wajibu wa kujenga bwawa hili katika mkataba wetu wa ukarabati wa barabara ya Arusha Minjingu lakini sisi kama kampuni tuna sera ya kujitoa kwa ajili ya matatizo ynayowakabili binadamu wenzetu”alisema Addi.
    Alisema zaidi ya msaada huo pia wananchi wa vijiji hivyo watapata hasa zile ambazo hazihitaji wataalamu kama sehemu ya kuwawezesha  kupata kipato.
     Aliongeza kuwa pia kampuni hiyo inaendesha pia mradi wa afya kwa kugharamia utoaji wa elimu ya ukimwi kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo pamoja na wananchi wa vijiji ambavyo barabara hiyo inapita.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages