Breaking News

Your Ad Spot

Jun 23, 2012

KUUA KATIKA UGOMVI KWENYE MCHEZO WA POOL KWA MPELEKA JELA MIAKA TISA

TARIME, TANZANIA
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, mjini ya Jaji Amir  Mruma imemuhukumu Mkazi wa Tarime  Chomete John Wambura kwenda jela miaka tisa baada ya kupatikana na hatia ya kuuwa bila kukusudia.
Katika kesi hiyo, Wambura amepatikana na hatia ya kumuua Chacha Ryoba Mkono kwa kumchoma kisu wakati wa ugomvi wakati  wakicheza  mchezo wa Pool.
Akitoa Hukumu hiyo Jumanne Wiki hii Jaji Mruma alidai kuwa amelidhika na Ushahidi uliotolewa Mahakamani hapo bila Shaka yoyote na Mtuhumiwa kuiomba Mahakama imsamehe kwani kosa lake la Kwanza na walikuwa wakigombea sh 200/= wakati wakicheza Pool ,
Ambapo ilidaiwa na  Mwanasheria wa Serikali Varence Mayega kuwa Mtuhumiwa Chomete alifanya Mauaji hayo  Agost 19/2009  Mchana katika Kijiji cha Genkuru tarafa ya Ingwe alipomchoma Mwenzake Chacha Ryoba Kisu wakati wakigombana na Kusababisha Kifo kwa Ryoba , mbali na Mtuhumiwa  kuiomba Mahakama  imusamehe kwa kuwa amekaa Mahabusu kwa mda mrefu Jaji Mruma alimuhukumu Kwenda Jela Miaka 9 ili iwe Fundisho kwa watu wengine wanaoondoa Roho za Watu bila Sababu za Msingi ,
Katika kesi nyingine katika Mahakama hiyo Kuu ya Jaji Mruma imemuhukumu Marwa Magembe naye kwenda Jela miaka 9 kwa kuuwa bila kukusudia , ambapo Mwanasheria wa Serikali Mayega alidai kuwa Matuhumiwa Magembe alimuuwa Murian Chacha Tugara usiku Agost 19 /2010 katika Kijiji cha Nyantira Tarafa ya Ingwe

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages