Breaking News

Your Ad Spot

Jun 15, 2012

MHARIRI WA GAZETI LA RAI KIZIMBANI KWA RUSHWA

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri
 Absalom Kibanda
Na Rose Jackson, Arusha
MHARIRI wa gazeti la Rai, Masiaga Matinyi ( 41) na wengine wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini Arusha wakikabiliwa na mashitaka kudaiwa kueomba rushwa ya sh. milioni 1.5 kutoka kwa Andrea Mahamud, mfanyakazi wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) wilayani monduli mkoani hapa.
     Akisomewa kesi hiyo  na waendesha mashataka, Rehema Mtota na Hamidu Msimbana  mbele ya hakimu Yohana Miyombo ilidaiwa kuwa watuhumiwa hao walifanya kosa hilo kati ya Juni 13 na 14 katika eneo la Monduli.
    Ilidaiwa katika kutenda kosa hilo walimshawishi,  Andrea Mahamud kutoa rushwa kwa kumtishia kwamba nafasi aliyonayo Tanesco haijakidhi vigezo vinavyohitajika.
    Aidha  mwendesha mashataka  aliwataja watuhumiwa wengine waliokuwa wamafuatana na mahariri huyo kuwa ni Mwita Chomete( 32 ambaye ni dereva wake  pamoja na Bora Bidiga (36) ambaye ni binti  aliyetoka nae Daar es Saalam  na kwamba kwa pamoja walifanya kosa hilo kwa pamoja huku wakijua ni kinyume cha sheria.
     Katika shitaka la pili ilidaiwa kwamba Juni 14,muda wa saa 10 jioni, Mwita Chomete alipokea kiasi cha sh. 200,000 kwa niaba ya mshitakiwa wa kwanza bw Matinyi kwa madai hayo hayo ya mwajiriwa huyo wa Tanesco kutokuwa na vigezo.
     Baada ya watuhumiwa hao  kusomewa mashataka hayo hakimu Yohana alitaja  masharti ya dhamana  kuwa ni  lazima mdhamini    kila mmoja awe anafanya kazi kwenye kamapuni inayofahamika na lazima asaini hati ya sh. 500,000 na hakukuwa na pingamizi ya dhama.
    upelelezi bado unaendelea ambapo  wahishtakiwa wawili wamepata dhamana huku  kesi hiyo ikihairishwa hadi juni 29 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages