Breaking News

Your Ad Spot

Jun 21, 2012

SBL YAZINDUA MRADI WA UVUNAJI MAJI YA MVUA IRINGA

 Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk. Leticia Warioba akizindua rasmi mradi wa uvunaji maji ya mvua uliopo Hospitali ya Wilaya ya Iringa iliyopo Frelimo mjini hapa jana. Mradi huo umefadhiliwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) na kugharimu zaidi ya Shilingi Milioni 50 na unataraji kuwanufaisha wakazi wa eneo hilo zaidi ya 100,000. Wengine kutoka kushoto ni Meya wa Manispaa ya Iringa, Amani Mwamwindi, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa SBL, Teddy Mapunda na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu, V Mushi.
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk. Leticia Warioba akimshukuru Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Teddy Mapunda kwa kampuni yake kufadhili mradi huo muhimu wa maji Hospitalini hapo.
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk. Leticia Warioba akifungua maji kutoka katika tanki moja wapo.
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk. Leticia Warioba akimtwisha ndoo ya Maji Augusta Mtemi ambaye ni Diwani wa Viti Maalum Iringa ikiwa ni ishara ya uzinduzi huo.
 Tanki litakalo tumika kusambaza maji katika mradi huo.

Hii ndio Hopspitali ya Frelimo iliyopo Manipaa ya Iringa ambayo itafaidika na mradi huo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages