Na Rose Jackson,Arusha
Shirika lisilo la kiserikali la Hope For Tanzania limetoa kompyuta 92 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 15 kama mchango wa kuinua kiwango cha elimu katika shule nne jijini Arusha.
Wakurugenzi wa shirika hilo hapa Tanzania Felex Masenge na Naomi Masenge wamesema kuwa msaada huo unatokana na wafadhili wa shule isiyo ya kiserikali ya Tuishime ambao waliahidi kuzisaidia shule 10 jijini arusha vifaa hivyo ili wanafunzi waweze kujifunza somo la Tehama.
Aidha bw Felex alisema kuwa zoezi hilo la kupatiwa computer linaendelea hali ambayo itatoa fursa kwa shule hizo kufanya vizuri kielimu katika ulimwengu wa sasa wa sayansi na teknolojia.
Akikabidhi computer hizo kwa wakuu wa shule hizo ambazo ni shule ya msingi uhuru,ukombozi,kijenge na tuishime mgeni rasmi katika hafla hiyo Afisa elimu vielelezo Godfrey Augustino alisema kuwa vifaa hivyo vimekuja wakati muafaka na amewataka kuvilinda na kuvitunza vizuri ili viweze kusaidia vizazi vinginevyo.
Pia alisema kuwa shule nyingi za serikali zinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa fedha hali ambayo inapelekea kushindwa kununua computer na wanafunzi kushindwa kufanya mitihani ya Tehama kama ilivyo kwa shule zinazomilikiwa na watu binafsi.
Aidha Augustino alitoa wito kwa wakuu hao wa shule kuzitunza na kuzilinda na kuwa hatokuwa tayari kupokea taarifa ya kupotea ama kuibiwa kwa vifaa hivyo bali hatua kali za kisheria zitachuliwa dhidi ya mwalimu husika.
Lakini hata hivyo amewataka walimu kwenda shule na kwenda kujifunza elimu ya computer ili waweze kuwafundisha wanafunzi somo hilo la Tehama na hatimaye waweze kufanya vizuri katika mitihani yao.
Akionge kwa niaba ya wakuu wa shule diwani wa kata ya sokon one Michael Kivuyo alisema kuwa ni vyema watanzania wakaiga mfano huo kwa kuchangia kuinua elimu katika shule za msingi na sio kuchangia ama kutoa msaada kwa mambo yasiyo ya msingi katika jamii.
Your Ad Spot
Jun 3, 2012
Home
Unlabelled
SHULE NNE JIINI ARUSHA ZAPATIWA KOMPYUTA ZENYE GHARAMA YA MILIONI 15
SHULE NNE JIINI ARUSHA ZAPATIWA KOMPYUTA ZENYE GHARAMA YA MILIONI 15
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269