Breaking News

Your Ad Spot

Sep 20, 2012

RAIS KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI DARAJA LA KIGAMBONI, DAR ES SALAAM


* Aonya 'wenye viwanda' vya kutunga uongo kuacha tabia hiyo na kuelekeza nguvu kwenye maendeleo
* Asema viongozi wa vyama vya upinzani badala ya kupigania maendeleo, wapo tayari nchi iyakose
*Asema tukio la kuwekwa jiwe la msingi ujenzi huo, leo litawanyima usingizi badala ya kufurahi

DAR ES SALAAM, TANZANIA
Rais Jakaya Kikwete leo, Alhamisi, Septemba 20, 2012, ameweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa Daraja la Kigamboni, Dar es Salaam, huku akiwaonya watu ambao amewaeleza kuwa wanavyo viwanda vya kutunga uongo kuacha tabia hiyo na kuelekeza nguvu kwenye maendeleo.

Aidha, Rais Kikwete amewahakikishia wakazi wote wa Kigamboni ambao wanaondolewa katika maeneo yao kwa ajili ya kupisha ujenzi wa daraja hilo na ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni kuwa watalipwa stahili na haki zao zote.

Daraja hilo la Kigamboni ambalo wazo la kujengwa kwake lilibuniwa kwa mara ya kwanza zaidi ya miaka 30, tokea mwaka 1978, wakati wa uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, linajengwa kwa gharama ya Sh. bilioni 214.6 na litakuwa tayari katika muda wa miezi 36 ijayo, ingawa muda huo unaweza kupungua na kubakia miezi 30.

Daraja hilo ambalo litakuwa na urefu wa mita 680 linagharimiwa kwa pamoja na Serikali na Shirika la Hifadhi ya Jamii la NSSF ambalo litachangia kiasi cha asilimia 60 na Serikali asilimia 40...INAENDELEA

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages