Breaking News

Your Ad Spot

Oct 16, 2012

MANONGI:TUACHE MALUMBANO TUJADILI HALI HALISI

Balozi wa  Kudumu wa Ubalozi wa Tanzania Katika Umoja wa Mataifa, Tuvako  Manongi, akizungumza  siku ya  Jumatatu,wakati wa Uzinduzi wa Tathmini ya Miaka  Minne ya Shughuli za Maendeleo za Umoja wa Mataifa ( QCPR). Uzinduzi ambao umefanyika  wakati wa Mkutano wa Baraza la Uchumi na Fedha  ( ECOSOC)la Baraza Kuu la 67 la  Umoja wa Mataifa. Tanzania ni Makamu Mwenyekiti wa  Baraza hilo.   Katika mchango wake Balozi aliwataka wajumbe wa mkutano huo kujadili hali halisi ya  matatizo ya kiuchumi , kuongezeka kwa umaskini na upunguaji wa misaada ya  kimaendeleo  kwa nchi  hasa  zinazoendelea na  nafasi ya  Umoja wa Mataifa katika  ufadhili na usimamiaji wa miradi ya mendeleo  badala ya nchi wanachama kutumia muda mwingi kujitafutia uhalali na umaarufu. Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Katibu  Mkuu, Bw. Jan Eliasson. HABARI KAMILI..BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages