Breaking News

Your Ad Spot

Oct 19, 2012

'WAISLAM' WACHAFUA TENA HALI YA HEWA DAR

DAR ES SALAAM, TANZANIA
Kama hali ilivyokuwa baada ya Sala ya Ijumaa iliyopita, leo baadhi ya waislam wanaotaka kujitambulisha kuwe wenye msimamo mkali hapa nchini wazua tafrrani katika maeneo mbali mbali ya jijini la Dar es Salaam na kusababisha hali ya amani kuwa ya wasi wasi.

Kufuatia tafrani hilo Daily Nkoromo Blog imeshuhudia maduka yakifungwa hasa  katika maeneo ya Kariakoo, ambako kwa kawaida huwa na pilikapilika nyingi za wafanya biashara kuliko maeneo mengi jijini Dar es Salaam.

Ilibidi polisi wa kikosin cha kuzuia ghasia kupambana na 'waislam' hao ambao awalifanya maandamano ya aina yake, kwa kuanza kukusanyika makundi madogo na maandaye kuwa makubwa ambapo polisi wamelazimika kutumia nguvu kuwatawanya.

Hadi sasa bado hali yaijarejea  kuwa shwari katika maeneo mbalimbali na polisi wanaonekana kuendelea kuimarisha ulinzi.

Yakijiri  zaidi tutawaletea baadaye

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages