Breaking News

Your Ad Spot

Nov 13, 2012

KIKWETE AJIUZULU UENYEKITI WA CCM, SAA 9;15, KUPISHA UCHAGUZI WA KUMPATA MWENYEKITI MPYA

 Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na Makamu wake wa Uenyekiti Dk. Amani Abeid Karume (Zanzibar) na Pius Msekwa (Bara) wakiondoka meza kuubaada ya kujiuzulu nafasi zao kufuatia kumaliza muda wao wa uongozi. Baadaye Kikwete ambaye ameteuliwa na CCM kugombea tena nafasi hiyo ya Uenyekiti alikaa upande wa wajumbe kushubiri kuchaguliwa tena. Tukio hili limefanyika saa 9:15 alasiri.
 Kikwete na meza kuu wakiwa upande wa wajumbe wa Mkutano Mkuu, wakati uchaguzi Mkuu kumpata Mwenyekiti mpya wa CCM Taifa ambapo yeye ni mgombea pekee.
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Benjamin Mkapa akiongoza Mkutano Mkuu kwa muda baada ya Kikwete kujiuzulu. Sasa mchakato wa upigaji kura kuchagua Mwenyekiti na kuwapata Makamu Wenyeviti Bara na Zanzibar unaendelea muda huu. FUatilia hapa kupata matokeo (Picha zote na Bashir Nkoromo)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages