MKUU
wa Wilaya ya Magu, Jacqueline Liana akizungumza jana (11.1.2013) na wafugaji wa
kata za Nyigogo na Kahangara wakati wa kufunga mafunzo ya ufugaji bora yaliyoendeshwa
kwa ushirikiano na Halmashauri ya Wilaya ya Magu na Kiwanda cha Kusindika Nyama
cha Alpha Choice LTD, kilichopo katika kijiji cha Bugabu, wilayani humo. Kulia
ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Naomi Nnko na kushoto ni Kaimu
Mkuu wa Idara ya Kilimo na Mifugo wa halmashauri hiyo, Dk. Kiraba Msoke.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Naomi Nnko, akizungumza jana
(11.1.2013) na washiriki wa mafunzo ya ufugaji bora kutoka kata za Nyigogo na
Kahangara yaliyofanyika katika kijiji cha Bugabu, wilayani humo. Kushoto ni
Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jacqueline Liana na kulia ni Kaimu Mkuu wa Idara ya
Kilimo na Mifugo katika halmashauri hiyo, Dk. Kiraba Msoke. Mafunzo hayo
yaliyoanza Januari 9, mwaka huu na kumalizika jana yaliandaliwa kwa ushirikiano
wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu na Kiwanda cha Kusindika Nyama (Picha zote na Emmanuel Ndege)
Your Ad Spot
Jan 12, 2013
Home
Unlabelled
DC MAGU AFUNGA MAFUNZO YA UFUGAJI BORA KATA ZA NYIGOGO NA KAHANGARA
DC MAGU AFUNGA MAFUNZO YA UFUGAJI BORA KATA ZA NYIGOGO NA KAHANGARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269