Breaking News

Your Ad Spot

May 21, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA 14 WA BARAZA LA USIMAMIZI WA MAWASILIANO AFRIKA, JIJINI DAR LEO


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam. Picha na OMR 
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongoza na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Prof. John Mkoma, wakati akiondoka kwenye chumba cha mkutano baada ya kufungu rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya washiriki wa mkutano huo.


Na Mwandishi Wetu


MAKAMU wa Rais Tanzania Bara, Dk. Mohammed Gharib Bilal, ameitaka sekta ya mawasiliano nchini kuhakikisha inakomboa wananchi kiuchumi, afya,kilimo na kielimu.

Bilal alisema kuwa huduma za kibenki na kutuma fedha zitasaidia kuondoa daraja lililokuwepo kati ya vijiji na mijini kutoka na huduma hizo kutumia mtandao ya simu.

Akizungumza leo katika ufunguzi wa mkutano wa 14 wa baraza la mawasiliano Afrika Dk. Bilal, alisema kuwa Serikali itahakikisha inatoa afya bora, maji salama ya kunywa na usafi wa mazingira, elimu, chakula na malazi,

Pia alisema kuwa itahakikisha inaboresha afya ya uzazi na kupunguza vifo vya watoto wachanga, kuwawezesha wanawake na wananchi wenye mazingira magumu zaidi ya jamii na kuhakikisha kunakuwepo na mazingira endelevu.

Dk. Bilal alisema mawasiliano ya makampuni katika Afrika yakifanya kazi kwa pamoja yatasaidia kuinua watu waishio vijijini na kutoa huduma bora ikiwemo kurahisisha upatikanaji wa mawasiliano na huduma za mtandao.

Mkutano huo umeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), na kuhudhuriwa na waziri wa Mawasiliano na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa na Mawaziri wa mawasiliano kutoka Sudan na Ghana.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages