Breaking News

Your Ad Spot

Jun 2, 2013

WATATU KUIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MASHINDANO YA KUOGELEA


Na Elizabeth John
CHAMA cha kuogelea Tanzania (TSA) kimechagua wachezaji watatu ambao wanatarajia kuliwakilisha taifa katika mashindano ya Dunia ambayo yanatarajia kuanza kutimua vumbi Julai 18 hadi Agosti 5 katika mji wa Barcelona nchini Hispania.
Wachezaji hao wanatarajia kuondoka nchini, Julai 17 chini ya kocha wao, Geofrey Kimimba ambaye atasaidiana na makocha wa wachezaji wanakotoka.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa TSA, Noel Kiunsi wachezaji hao ni Hilal Hilal, Ammaar Ghadiyali na Mariam Foum.
“TSA tulikutan ana kuchagua wachezaji ambao tunauhakika wataenda kuitangaza nchi yetu vizuri, hivyo tunaukhakika na wachezaji hao, tuwaombee kwa mungu wafanye vizuri,” alisema Kiunsi.
Alisema wachezaji hao pamoja na wenzao wanaendelea na mazoezi ya kujiweka sawa kwaajili ya kushiriki mashindano hayo katika bwawa la chuo kikuu cha Dar es Salaam.
 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages