Breaking News

Your Ad Spot

Jun 2, 2013

CHIKU AISAMBAZA 'SAUTI YAKE'


Na Elizabeth John
MWANADADA ambaye anatesa katika tasnia ya muziki wa hip hop, Chiku Keto, ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Sauti yangu’ ambao umeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.
Mbali na kutamba na kibao hicho, mwanadada huyo alishawahi kutamba na kibao chake cha ‘Fahari ya Kusini’ ambacho kilifanya vizuri na kumuweka pazuri msanii huyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Chiku aliwataka wapenzi wa kazi zake wakae mkao wa kula kwaajili ya kuzipokea kazi zake nyingine zinazofuata ikiwa ni pamoja na video ya ngoma hiyo.
“Najua kazi hii itapokelewa vizuri na mashabiki wangu, kwasababu mashairi niliyotumia ndani yake yamesimama kisanii hivyo naomba sapoti yao,” alisema Chiku.
Mwanadada huyo ni kati ya wasanii ambao wanafanya vizuri katika tasnia hiyo, anaomba wapenzi wake wakae mkao wa kula kwaajili ya kuvipokea vitu vizuri kutoka kwake.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages