NA CHIBURA MAKORONGO, SHY
UCHAGUZI wa Naibu meya katika Manispaa ya Shinyanga umefanyika jana ikiwa Davidi Nkulila (CCM) diwani kata ya Ndembezi amerudia kuongoza kiti hicho kwa kupata kura 14 zilizopigwa na wajumbe hao kati ya kura 22 huku mpinzani wake Nyangaki Shilungusheila (CHADEMA) diwani kata ya Kambarage akiambulia kura nane
.
Katika uchaguzi huo ulioongozwa na mstahiki meya Gullamu Hafidhi Mkadamu akiwepo na mkurugenzi wa manispaa hiyo Festo Kang’ombe uliofanyika ndani ya ukumbi wa mkoa mara baada ya kumaliza kikao cha bara za la madiwani huku zikiundwa kamati mbili za kudumu.
Hata hivyo kamati hizo ambazo ni kamati ya afya,elimu,uchumi na fedha ambapo mwenyekiti wake Charles Njage ( CCM)diwani wa kata ya Kizumbi alichaguliwa kwa kupigiwa kura na wajumbe waliokuwa ndani ya kamati hiyo.
Aidha katika upande wa kamati ya miundombinu mwenyekiti alichaguliwa Thomas Chuma (CCM) diwani wa kata ya Lubaga huku wajumbe wengine wakiendelea kuchaguliwa kuwemo ndani ya kamati mbalimbali zilizopo.
Pia Nkulila aliwashukuru wajumbe kwa kumpatia kura za kurudi tena katika uongozi kwa nafasi hiyo na kuwaahidi ushirikiana kama alivyokuwa akifanya siku zote katika uongozi huo huku shilungushela akikubali matokea hayo.
Alisema katika uongozi wake hapendelei mambo ya siasa katika vikao vya kwenye baraza la madiwani bali kinachotakiwa ni kuwa kitu kimoja cha kuwawakilisha wananchi matakwa yao walivyoyaagiza kuhusu siasa ni nje mara baada ya kikao kumalizika.
Hata hivyo madiwani hao walipongeza uchaguzi huo ulikuwa wa uhuru na haki, ikiwa mwanasheria wa manispaa hiyo James Mwakinya akisoma vifungu vya kanuni na sheria vya uchaguzi huo kuwa uchaguzi huo ni wa haki kwa kila mwaka kumpata naibu au makamu mwenyekiti ndani ya manispaa.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269