Breaking News

Your Ad Spot

Sep 23, 2013

POLISI WATATU WAFARIKI, NANE WAJERUHIWA KATIKA AJALI YA GARI WAKITOKA KATIKA OPERESHENI KIMBUNGA

Na Chibura Makorongo,Kahama 
POLISI watutu wa wa mkoa wa Njombe wamekufa na wengine wanane kujeruhiwa wakiwemo maofisa uhamiaji baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka katika kijiji cha Malenge  wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga.
Ajali hiyi imetokea ikihusisha gari lenye namba PT 0762 aina ya Landrover 110 kupinduka jana saa 12:00 jioni lilipokuwa likitokea mkoani Kagera katika operesheni Kimbunga ya kuwaondoa wahamiaji haramu  ambapo lilikuwa njiani kurudi mkoani Njombe.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Kihenye Kihenya alisema  marehemu hao walitambulika kwa jina moja kuwa ni PC Marco wa kituo cha polisi Njombe,  D-CPL Fredy  pamoja na PC Sufiani wote wa kituo cha polisi Makambako.
Aidha kaimu kamanda aliwataja majeruhi ambao ni askari polisi kuwa ni Pc Hussein aliyepata jeraha kichwani pamoja na mguu wa kushoto na hali yake inalezwa kuwa ni mbaya ambapo hadi sasa hajazinduka,  Inspekta Leornad aliyemia kiuno, PC Yusuph ambaye ndiye dereva wa gari hilo aliyeumia kiuno wote kutoka kituo cha Njombe.
Wengine ni  DC Lambuli aliyeumia paji la uso pamoja na mguu wa kulia, PC James aliyeumia goti pamoja na mkono wa kushoto pamoja na PC Adamu aliyeumia paji la uso nao kutoka kituo cha polisi cha Njombe.
Maafisa uhamiaji waliokuwemo kwenye ajli hiyo aliwataja kuwa ni Glory Temu kutoka mkoa wa Mbeya na inaelezwa kuwa hali yake ni mbaya ambapo hadi sasa hajapata fahamu pamoja na Augustino Nanyambe kutoka mkoa wa Rukwa aliyeumia goti pamoja na mkono wa kushoto.
Kamanda Kihenya alisema kuwa miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama huku pia majeruhi hao wakipatiwa matibabu katika hospitali hiyo na kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo hakijafahamika ambapo polisi bado wanaendelea na uchunguzi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages