Breaking News

Your Ad Spot

Sep 13, 2013

SERIKALI: HATUFUKUZI WAKIMBIZI BALI WAHAMIAJI HARAMU

NA MAGRETH KINABO –MAELEZO
SERIKALI imesema kwamba haijawafukuza wakimbizi nchini huku ikitoa ufafanuzi kuwa zoezi linaloendelea hivi sasa linahusiana kuwabaini na kuwarejesha kwao wahamiaji haramu ambao wamekuwa wakiishi hapa nchini kinyume cha sheria.

 Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Isaac Nantanga kufuatia  vya habari vya nje ya nchi kutangaza kuwa  Serikali ya Tanzania imewarudisha kwao kwa nguvu wakimbizi 25,000 kutoka nchi ya Burundi katika kipindi cha muda wa mwezi mmoja uliopita.

“ Hakuna  mkimbizi yeyote aliyerudishwa Burundi ,kwa hiari wala kwa nguvu katika kipindi kilichotajwa. Kipindi cha mwisho cha kuwarejesha wakimbizi kwa hiari kilikuwa mwaka 2012,ambapo hadi Desemba mwaka huo wakimbizi 34,000 kutoka Burundi waliokuwa katika kambi ya Mtabila, iliyoko Kigoma walirejeshwa  makwao kwa hiari kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi(UNHCR) na  Serikali ya Burundi,” alisema Nantanga.
 Alisema Serikali Tanzania   bado inaendelea kuwapa hifadhi wakimbizi kuendelea kuishi kwenye kambi na makazi yaliyopo hapa nchini, ambapo jumla ya wakimbizi 264,000 wanapata hifadhi.

“Hadi leo wapo wakimbizi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo  ( DRC)  wapatao 64,172 kwenye kambi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, wakimbizi 175,473  kutoka Burundi wapo kwenye makazi ya wakimbizi ya Mishamo na Katumba wilayani, mkoa wa Katavi na Bulyankulu mkoani Tabora.

Pia wamo wakimbizi 2,128 kutoka Somalia kwenye makazi ya Chogo wilayani Handeni,Tanga, wakimbizi 22,227 kwenye wilaya ya Kasulu na Kigoma vijijini.

Taarifa hiyo    ilifafanua kwamba vyombo  zoezi la kuwarudisha wahamiaji hao lilianza Agosti mwaka huu. Lakini kabla ya hapo walipewa muda wa wiki mbili kurejea kwao kwa hiari ama kupata vibali halali vya kuwawezesha kuendelea kuishi hapa nchini.
“Hadi Septemba 4, mwaka huu zaidi wahamiaji haramu 27,000 walikuwa wamerejea  kwao kwa hiari. Wahamiaji hawa haramu walikuwa katika mikoa ya Kagera, Kigoma na Rukwa.

Baada ya  muda waliopewa wa kuondoka au kujisajili  kihalali kuisha, Serikali sasa imeaanza operesheni ya kuwabaini wahamiaji hao waliokaidi wito wa kuwataka kuondoka kwa hiari ,” alisema Nantanga.

 Nantanga aliongeza kuwa operesheni hiyo inafanywa kwa uangalifu mkubwa ili kuhakikisha kuwa  wanaokamatwa na kurejeshwa kwao ni wahamiaji haramu kweli na sio raia au wageni wenye hati halali za kuishi hapa nchini.

Aidha alisema Serikali inatoa wito kwa vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi kushirikiana  na Serikali kutoa taarifa sahihi kwa kuwasiliana na mamlaka husika pale wanapopelekewa taarifa zenye utata.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages