Breaking News

Your Ad Spot

Sep 11, 2013

TIGO YAGAWA BAJAJI KWA WASHINDI WA DROO YA NANE YA PROMOSHENI YAKE

 Mshindi wa droo ya 8 katika promosheni ya Tigo 'Miliki Biashara Yako' Bi. Julieth Weria (25) mkazi wa Kigamboni akionyesha ufunguo wake wa Bajaji kwa furaha mara baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo na Meneja Bidhaa wa Tigo Bw. Husni Seif (kushoto) katika hafla fupi ya makabidhiano yaliyofanyika Kimara Mwisho jijini Dar es Salaam.
 Meneja Bidhaa wa Tigo Bw. Husni Seif (kushoto) akimuelekeza mshindi wa promosheni ya ‘Miliki Biashara Yako’ wa droo ya 8  Bw. Meshack Ndoje (28) ambaye ni mwanafunzi wa UDSM jinsi ya kuwasha Bajaji yake mpya yenye thamani ya Tsh 6,700,000 katika hafla ya makabidhiano yaliyofanyika Kimara Mwisho jijini Dar es Salaam.
 Mshindi wa droo ya 8 katika promosheni ya Tigo ‘Miliki Biashara Yako’ Bw. Godwin Kajala (34) ambaye ni mfanyabiashara wa vipodozi  na mkazi wa Kimara akijaribu Bajaji yake mpya aliyokabidhiwa na Tigo wakati wa hafla fupi ya makabidhiano yalifanyika Kimara Mwisho, jijini Dar es Salaam. Pembeni yake ni Meneja Bidhaa wa Tigo Bw. Husni Seif akimkabidhi ufunguo wa Bajaji.
 Meneja Bidhaa wa Tigo Bw. Husni Seif akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa makabidhiano ya Bajaji kwa washindi wa droo ya 8 ya promosheni ya ‘Miliki Biashara Yako’ iliyofanyika Kimara Mwisho jijini Dar es Salaam.
 Mshindi wa droo ya 8 katika promosheni ya Tigo ‘Miliki Biashara Yako’ Bw. Elinaza Mbaruku (kushoto) ambaye ni mkulima na mfugaji wa kuku wa nyama akipokea ufunguo wa Bajaji yake mpya kutoka kwa Meneja Bidhaa wa Tigo Bw. Husni Seif wakati wa hafla fupi ya makabidhiano yalifanyika Kimara Mwisho, jijini Dar es Salaam.
Mshindi  wa droo ya 8 katika promosheni ya ‘Miliki Biashara Yako’ Bw. Meshack Ndoje (28) ambaye ni mwanafunzi wa UDSM akipungia kwa furaha kutoka ndani ya Bajaji yake yenye thamani ya Tsh 6,700,000 wakati wa hafla fupi ya makabidhiano yaliyofanyika Kimara Mwisho jijini Dar es Salaam. Akitazama ni Meneja Bidhaa wa Tigo Bw.Husni Seif.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages