Breaking News

Your Ad Spot

Oct 28, 2013

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MZIZIMA WAHAMASISHWA KUJIUNGA KLABU ZA UMOJA WA MATAIFA

DSC_0083
Mgeni rasmi Balozi wa Hispania nchini, Luis Manuel Cuesta Civis akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mzizima umuhimu wa kujiunga na vilabu vya vijana unaoratibiwa na Umoja wa Mataifa katika ngazi za shule za msingi na sekondari wakati wa maadhimisho ya siku ya Umoja wa Mataifa yaliyoandaliwa na shule hiyo.
DSC_0297
Afisa Habari wa Kitengo cha Mawasiliano cha Umoja wa Mataifa, Usia Nkhoma Ledama akizungumza vijana wa Shule ya Sekondari ya Mzizima katika kampeni ya kuwahamasisha vijana wa shule za sekondari kujiunga na vilabu vya vijana ili waweze kupata nafasi ya kujifunza malengo ya milenia, mijadala, program za redio ili kukuza uelewa wao kuhusu umoja wa mataifa
Umoja wa Mataifa kufanya kazi kwa karibu na vijana wa Tanzania katika ngazi ya shule za msingi, sekondari na vyuo kupitia Vilabu vya Umoja wa Mataifa. Vilabu na wajumbe wa wanafunzi wa shule za sekondari ambao kujipanga ili kuongeza uelewa na ufahamu msaada wa Umoja wa Mataifa.
Vilabu vya Umoja wa Mataifa katika ngazi ya chuo kikuu ni inayojulikana kama Sura ya Umoja wa Mataifa. Hivi sasa kuna vilabu 221 vya Umoja wa Mataifa katika Tanzania Bara na Zanzibar.
Mtandao wa Vilabu wa Umoja wa Mataifa , Umoja wa Mataifa Vilabu Mtandao Tanzania ( UNCTN ), ilianzishwa mwaka 2006 . UNCTN inatoa jukwaa kwa njia ambayo Vilabu vya Umoja wa Mataifa ni kuletwa pamoja na jukumu katika masuala ya maendeleo zinazoikabili Tanzania kwa ujumla, na wale ambayo kuathiri vijana hasa.
Vilabu huwapa wanafunzi nafasi ya kupanga na kushiriki katika shughuli za baada ya shule ambayo ni pamoja na: kuwafikia, upendo kazi na matukio ya Umoja wa Mataifa -kuhusiana na jamii kama vile kuongeza ufahamu juu ya Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) , mijadala , programu za redio na mikutano Club. Vilabu pia kuruhusu vijana kushiriki katika mafunzo , warsha na mikutano ya ndani na nje ya nchi , hasa katika ngazi ya kitaifa , kikanda na kimataifa Model Mkutano wa Umoja wa Mataifa .
DSC_0166
Mwenyekiti wa UN Chapter chuo kikuu cha Dar es Salaam Bw. Pascal Mashanga akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Mzizima kuwahamasisha kujiunga na vilabu vya Umoja wa Mataifa na faidi zake hapo baadae wakati wa sherehe maalum ya siku ya Umoja wa Mataifa iliyoandaliwa na shule hiyo.
DSC_0091
Picha juu na chini ni Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Mzizima wakionyesha furaha katika siku hiyo maalum iliyoandaliwa na shule yao.
DSC_0094
DSC_0064
DSC_0217
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mzizima wakitoa buradani mbalimbali wakati wa siku maalum ya kusheherekea maadhimisho ya Umoja wa Mataifa kwa mila na desturi za tamaduni tofauti kama inavyoonekana pichani.
DSC_0137
DSC_0192
DSC_0127
Baadhi ya vijana wa shule ya sekondari ya mzizima wakifuatilia burudani mbalimbali wakati wa tukio hilo.
DSC_0131
DSC_0155
Mwalimu Rebeca Llavata wa shule ya sekondari Mzizima (aliyenyoosha mkono) akiteta jambo na Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, Usia Nkhoma Ledama wakati maadhimisho ya siku ya Umoja wa Mataifa yaliyoandaliwa na shule ya Sekondari Mzizima ya jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha.
DSC_0316
Usia Nkhoma Ledama akizungumza na moja ya klabu ya vijana shuleni hapo.
DSC_0337
Baadhi ya wanachama wa UN Club wa shule ya Sekondari Mzizima wakimsikiliza kwa makini Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa Usia Nkhoma Ledama (hayupo pichani).
DSC_0351
Mlezi wa UN Club akifafanua namna atakavyoweza kuendesha shughuli mbalimbali kupitia Club hiyo ili kuwajenga kidiplomasia wanafunzi wake.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages