Breaking News

Your Ad Spot

Dec 23, 2013

ASKOFU ATAKA WATENDAJI WA NGAZI ZA CHINI NAO WAWE WANACHUNGUZWA SAMBAMBA NA KUWAJIBISHWA MAWAZIRI

Na Chibura Makorongo, Shinyanga
ASKOFU Edson Mwombeki  wa kanisa la Emanuel  ameiomba tume itakayoundwa na Rais Jakaya  Kikwete  ichunguze kwa kina  watendaji  wa chini ambao  wamesababisha  kupoteza sifa ya uongozi wa mawaziri wanne kwa kufanya kazi kwa mazoea hivyo kuifanya serikali ichukiwe na wananchi.

“Sababu tumeanza kupoteza viongozi ambao walikuwa wanaonyesha uzalendo katika utendaji wa kazi kwa mfumo uliopo kwa sasa au tabia, Rais asipokuwa makini kutaendelea kuchagua  mawaziri na kuwawajipisha  kutokana na utendaji mbovu  kutoka ngazi za chini wanaofanya kazi kwa  mazoea”, alisema  Askofu Mwombeki.

Askofu huyo aliyasema hayo mbele ya  waumini wa kanisa hilo  baada ya kuisha ibada ya siku ya jumapili  huku akiwataka watanzania wote kuiombea nchi hii kwa kudumisha  maombi na amani kwani ndio njia pekee ya kuliletea sifa na utukufu taifa la Tanzania.

Hivyo aliwaomba wabunge waangalie  utendaji wao wa kazi  na katika maamuzi kwani wengine maamuzi yao ndani yake kuna wivu, lakini pia  Rais pindi anapounda tume ya kuchunguza tuhuma zilizoelezwa na kamati mbalimbali ndani ya bunge tume ielekezwe kuchunguza kwa kina watendaji wa chini ambao wamesababisha kupoteza mawaziri kama hao wanne kwa kufanya kazi  kwa mazoea na kuifanya serikali kuchukiwa na wananchi.

“Kitendo cha utendaji mbovu na wamazoea kinamfanya Rais akae  na kuwazia kuunda au kuvunja  baraza la mawaziri, huku akimtaka waziri mkuu  kujipima kwa kunagalia utendaji wa halmashauri  ambao umekuwa na ubadhirifu  wa fedha za umma,vitengo vyingi  vya serikali ngazi ya chini  amekosekana mtu wa kukemea  hivyo watanzania wanakosa imani na utendaji wa aina hiyo”alisema  Askofu  Mwombeki.

Alisema imeelezwa  wakurugenzi 52 na watumishi zaidi ya 60  katika halmashauri mbalimbali wanatuhumiwa kwa ubadhirifu wa matumizi mabaya ya fedha za umma  pia kuwepo na tuhuma  nyingi za  ujenzi wa miradi chini ya viwango na kufanya kila kikao cha bunge  kupiga kelele ambapo imekuwa ni jambo la kusikitika kama watanzania  na mali kutafunwa hovyo.
 
Aidha  alisema kuwa   mawaziri wamebeba  msalaba kama yesu  alivyoteswa msalabani kwa kuvikwa mataji ya miba  na kugongelewa misumari kwaajili ya dhambi za mwanadamu  hivyo hivyo akiwafananaisha  mawaziri kutuhumiwa kwa makosa yanayofanywa na baadhi ya wananchi wakiwemo watendaji wa serikali  kwa kukosa upendo wa moyoni na kukiuka haki za kibinadamu.

Kweli baada ya  Rais  kutengua baraza la mawaziri mwaka jana  na kuunda upya  kulionekana mabadiliko makubwa katika utendaji  ambao ulileta uthibiti mkubwa   hasa katika wizara ya maliasili na utalii huku akionyesha utendaji wake mkubwa  na umakini  ila mfumo uliomuangusha ni utendaji kazi kwa ngazi ya chini kwa mazoea mfumo huo usipo kemewa kwa nguvu  Tanzania itaendelea kupoteza  mawaziri na kuwawajibisha kwa utendaji uliopo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages