Breaking News

Your Ad Spot

Dec 25, 2013

MSICHANA AMUUA MPENZI WAKE KWA KUMVUTA KORODANI

MEATU, Simiyu, Tanzania
Mkazi wa kijiji cha Usiulize wilayani Meatu mkoani Simiyu anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumuua mpenzi wake kwa kumvuta korodani kutokana na wivu wa kimapenzi.
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu kamishina msaidizi mwandamizi Charles Mkumbo aiambia theNkoromo Blog kuwa tukio hilo lilitokea jana saa tisa usiku katika kitongoji cha mlimani kijiji cha Usiulize kata ya Mwamalole wilayani Meatu.
 
Alisema katika tukio hilo wapenzi wawili Jumanne Gunda (39) mkazi wa kijiji cha Kinyambuli wilayani Mkaramo wakiwa wamelala na mchumba wake Mariamu Khamis (49) mkazi wa kijiji cha Ibaga wilaya ya Mkaramo mkoani Singida ilitokea kutoelewana kati yao na kusababisha wagombane.
 
Katika ugomvi huo ambao chanzo chake ni wivu wa kimapenzi Mariamu alifanikiwa kuzivuta korodani za mpenzi wake na kusababisha mishipa muhimu kukatika na kusababisha kifo cha mpenzi wake Jumanne papo hapo.
 
Kufuatia kifo hicho Mariamu aliuburuza mwili wa mpenzi wake mpaka chooni kwa lengo la kuudumbukiza katika shimo la choo lakini hata hivyo kutokana na udogo wa tundu la choo alishindwa kuudumbukiza mwili huo chooni na hivyo kuamua kuutelekeza humo humo.
 
Asubuhi kulipopambazuka majirani wa nyumba waliyokuwa wamefikia wapenzi hao waliugundua mwili wa marehemu ukiwa umetelekezwa chooni na kutoa taarifa katika kituo cha polisi ambao walifika katika eneo la tukio na kumtafuta mtuhumiwa Mariamu.
 
Baada ya kukamatwa kwa Mariamu alikiri kumuua mpenzi wake katika ugomvi kati yao uliotokea usiku walipokuwa wamelala wote wawili ambapo alikiri kumvuta korodani zake na kusababisha kifo chake.
 
Kamanda Mkumbo alisema katika tukio lingine juzi majira ya saa 2.30 usiku huko katika kijiji cha Itubukilo kata ya Ngulyati wilaya ya Bariadi mwanamke mkulima wa kijiji hicho, Thereza Mtobangi (67) alitoka nje ya nyumba yake kwenda kujisaidia na wakati akirudi alidakwa na fisi aliyemshambulia aliyemburuzia kichakani ambako alimshambulia sehemu mbalimbali za mwili wake na kusababisha kifo chake.
 
Mjukuu wa marehemu aliyekuwa amemsindikiza Leah Maduhu (11) alipiga kelele za kuomba msaada kutoka kwa majirani baada ya bibi yake kukutana uso kwa uso na fisi huyo na majirani walipojitokeza walianza msaka na kufanikiwa kumkurupusha fisi akiwa vichakani akiwa ameisha muua bibi yake.
 
Hata hivyo majirani hawakufanikiwa kumkamata fisi huyo baada kuwahi kukimbilia vichakani ambako hivi sasa wanakijiji kwa kushirikiana na maofisa maliasili wanaendelea kumsaka fisi huyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages