Breaking News

Your Ad Spot

Jan 17, 2014

TAARIFA YA CAG YAMNG'OA MEYA MANISPAA YA BUKOBA

LUDOVICK UTOUH
BUKOBA, Tanzania
Meya Wa Manispaa ya Bukoba Antory Amani amejiuzuru nafasi hiyo baada ya Waziri mkuu Mizengo Pinda kumtaka Meya huyo kujipima mwenyewe au  kujiuzuru na akikaidi  baraza la madiwani wachukue hatua ya kumwajibisha kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye.
Hali hiyo imetokea baada ya taarifa ya Mkaguzi na Mthibiti Mkuu wa Hesabu za Serikalia Ludovick Utouh, kutoa taarifa yake  leo juu ya ukaguzi uliofanywa katika Manispaa hiyo kwa muda wa siku 35 na kubaini tuhuma zaidi ya 30  zilizokuwa zikimkabiri Meya wa huyo  pamoja na baadhi ya watendaji wa Manispaa hiyo pamoja na mkurugenzi wa Manispaa hiyo na  aliyekuwepo wakati huo Hamisi Kaputa.
“Nimeafiki na kukubali maamuzi ya na maelekezo yaliyotolewa na Serikali  mimi ni mtu mzima nimejiuzuru” alitamka amani kwa ufupi.
Akitoa taarifa hiyo  ya ushauri huo katika kikao kilichofanyika mjini Bukoba katika ukumbi wa mikutano wa mkuu wa mkoa wa Kagera kwa niaba ya Waziri mkuu, Naibu Waziri wa Tamisemi Agrey Mwanry,  alisema kuwa baada ya tuhuma juu ya makosa mengi ya kiutendaji ikiwemo  matumizi mabaya ya fedha ya umma, kusaini mikataba kinyume bila kuwashirikisha baraza la madiwani na kuikosesha mapato Manispaa hiyo kwahiyo ameamu kutoa magizo hayo.
Aidha amemtaka mkurugenzi aliyekuwa katika Manispaa hiyo kwa  kipindi hicho Hamis Kaputa ambaye alihamishiwa katika Halmashauri mpya ya ya Wilaya Momba mkoani Mbeya baada ya kuzuka kwa mgoro kati ya madiwani na uongozi wa Manispaa hiyo kuvuliwe wadhifa huo mara moja huku maafisa watatu ndani ya wa Manispaa hiyo waliohusishwa na tuhuma hizo kuvuliwa nyadhifa zao ambao ni Steven Nzihirwa ambaye ni mhandisi wa Manispa hiyo,Baraka Marwa ambaye ni afisa manunuzi na mhekazina Amduni Ulomi aliyekuwepo wakati huo ambaye inadaiwa kuwa yuko masomoni nje ya mkoa huu.
Aliagiza kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani katika Halmashauri hiyo kiimalishwe ili kiweze kufanya kazi ipasavyo na  pia itaundwa kamati ambayo itashirikiana na Seriakali za mitaa kufanya wa ukaguzi wa mambo mengine ambayo yamebainika kuhitaji ukaguzi zaidi kikiwemo uuzwaji wa kiwanja cha michezo  cha shulea ya msingi Kiteyagwa ambapo maagizo hayo yanapswa kutelelezeka ndani ya wiki moja na kutoa taarifa katika ofisi ya Waziri mkuu juu ya utekelezaji wa maagizo yake.
Baadhi ya miradi iliyokuwa ikibishaniwa na madiwani wa Manispaa ya Bukoba kuwa haikufuata taaratibu za kisheria kuwa ni ujenzi wa soko kuu la Bukaba,ujenzi wa kituo cha mabasi Kyakailabwa,mradi wa viwanja 5000 na viwanja 800,mradiwa ujenzi wa kituo cha kuoshea magari cha machinjioni,Meya kusaini mkopo wa mil.200 bila kufuata utaratibu na kutofuata taratibu wa kuwapata wakandarasi na kutowashirikisha wa  madiwani wa manispaa hiyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages