Breaking News

Your Ad Spot

Jan 6, 2014

WALIOKUFA KATIKA AJALI YA MELI ZANZIBAR WATAMBULIWA

NA MWANDISHI WETU ZANZIBAR
ABIRIA waliokufa katika ajali ya boti ya Kilimanjaro 11, mali ya Kampuni ya Azam Marine iliyokuwa ikisafiri kutokea Pemba kwenda Unguja wametambuliwa.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Zanzibar, Abdi Maalim  (PICHANI) amewataja marehemu hao kuwa ni Nashra Khamis Issa (10) na kaka yake, Ikram Khamis Issa (11),
Rashid Said Ali (11), Masoud Hamad Abdalla (30) na Fatma Khamis (18).

Maalim pia aliwataja majeruhi walionusurika katika ajali hiyo kuwa ni Alia Maulid Haji (19), Ali Salim Ali (22) na  Nahri Ali Issa (22), ambao alisema  wametibiwa na kuruhusiwa.

Ajali hiyo ilitokea baada ya boti hiyo kukumbwa na dhoruba katika eneo la Nungwi, Unguja, hali iliyosababisha hofu miongoni mwa abiria wake na wengine kuamua kujitosa baharini ili kuruhusu maisha yao lakini wengi wao walisalimika baaada ya kuokolewa.

Katika hatua nyingine, Maalim amesema hadi jana saa saba mchana hakuna maiti wala majeruhi waliopatiakana kutokana na msakao wa uopoaji na uokoji ulioendelea katika maeneo mbalimbali, yakiwemo ya kisiwa cha Nungwi.

"Boti mbili za wananchi wa Nungwi, KMKM, Polisi na tagi za Bandari ambazo zimetafuta zaidi upande wa baharini  zimerejea bila kupata mtu au mwili isipokuwa zimekuta viloba vikielea"  alisema.,

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages