Breaking News

Your Ad Spot

Feb 21, 2014

PSPF YAWAPIGA MSASA WANAHABARI DAR, WENGI WAVUTIWA WAJIUNGA NA MFUKO HUO

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu akiaga baada ya kumalizika kwa semina aliyowaandalia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu utendaji wa mfuko huo pamoja na kuwahamasisha kujiunga nao. Waliohudhuria semina hiyo ni wachora katuni, wamiliki wa mitandao ya kijamii na wahabari kutoka vituo vya televisheni, redio na magazeti.
 Ofisa wa PSPF akiwaelekeza baadhi ya wanahabari kujza fomu za kujiunga na mfuko huo katika mfumo wa hiari ambapo kiingilio ni sh. 10,000.
 Wanahabari wakiwa katika semina hiyo
Wadau
 Wanahabari wakiwemo wamiliki wa mitandao ya kijamii wakishiriki katika semina hiyo
Wadau
  Wanahabari wakiwemo wachora katuni wakihudhuria semina hiyo
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa PSPF, Masha Mshomba akifafanua jambo wakati wa semina hiyo.
 Meneja Mawasiliano na Masoko wa PSPF, Costantina Martin akielezea utaratibu wa kujiunga na mfuko huo
 Wamiliki wa mitandandao ya kijamii (Bloggers) wakiwa katika semina hiyo
 Meneja Uchangiaji wa Hiari wa PSPF, Mwanjaa Sembe akielezea umuhimu wa wanahabari kujiunga na mpango huo.
 Mkurugenzi wa  Mipango na Uwekezaji akitaja baadhi ya miradi waliyowekeza
 Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu akijibu baadhi ya maswali ya wanahabari

 Mwandishi wa Habari mkongwe wa magazeti ya Serikali Daily News na Habari Leo, akitoa neno la shukurani kwa PSPF baada ya kumalizika kwa semina hiyo.
 Mtunza Kumbukumbu wa PSPF, Lonick Nkinda akielezea mpangilio wa kuhifadhi kumbukumbu  za wateja kwa njia ya kisasa.
 Nkinda akionesha moja ya faili la mteja
 Meneja wa Huduma kwa Wateja wa mfuko huo, Laila Maghimbi akitoa maelezo kwa wanahabari kuhusu mashine zinazotoa namba kwa mteja inayomwelekeza dirisha la kwenda kuhudumia katika Makao Makuu ya PSPF, Dar es Salaam.
 Wanahabari wakipata maelezo kuhusu kitengo cha kuhudumia wateja kwa simu (Call Centre) kinachotarajiwa kuanza  kutoa huduma hivi karibuni.
Wateja wakihudumiwa katika kitengo cha Huduma kwa Wateja Makao Makuu ya PSPF, Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages