Breaking News

Your Ad Spot

Feb 13, 2014

RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI AIFAGILIA TAASISI YA AGA KHAN KWA KUSAIDIA MAENDELEO YA JAMII

DAR ES SALAAM, Tanzania
RAIS Mstaafu wa awamu ya pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi ameipongeza Taasisi ya Aga Khan kwa kuwa mstari wa mbele katika kusaidia Jamii ya Watanzania kimaendeleo

Pia, amesema maonyesho ya Aga Khan yanayoendelea kufanyika nchini yanaonyesha ushirikiano wa dhati uliopo baina ya taasisi hiyo na Tanzania.

Mwinyi (picahni juu), aliyasema hayo jana jioni, alipotembelea maonyesho hayo huku akiwa ameambatana na Waziri Mkuu Mstaafu, Samwel Malicela, alisema taasisi yab Aga Khan imefanya mambo mengi nchini.

Alisema binafsi amebahatika kukutana na Imam Aga Khan zaidi ya mara mbili, ambapo zote amekuwa akizungumza mambo mengi ya maendeleo kuhusiana na Tanzania.

"Imam Aga Khan muda wote amekuwa na akisisitiza maslahi na mafanikio ya watanzania hayo yanatokana na kuwa na mapenzio mema na watanzania,''alisema.

Alisema jambo hilo ndio maana lilimfanywa kuwa mstari wa mbel katika kuboresha sekta ya elimu na afya, ambayo imekuwa tegemeo kubwa la watanzania kunufaika na huduma hizo.

Hivyo, alisema maonyesho hayo yameonyesha ni namna gani Aga Khan amekuwa akiisaidia nchi bila kujali dini, rangi au kabila yeye anachojari ni utu.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Taasisi ya Shia Ismailia Tanzania, Kamal Khimji alisema maonyesho hayo wanayatumia kuonyesha upendo na namna gani wanavyojitahidi kuisaidia wananchi
 Rais Mstaafu wa awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi akikaribishwa katika hafla ya Maonyesho ya picha kuhusu Taasisi ya Aga Khan, jana kwenye ukumbi wa Diamod Jubilee jijini Dar es Salaam.
Mzee Mwinyi akisalimia viongozi mbalimbali wa taasisi hiyo
Mzee Mwinyi akiendelea kusalimia 
Salam
Salam
Salam na viongozi
Salam na viongozi
Salam na viongozi
Mwisho wa salam na viongozi
Sheikh Mkuu Mufti wa Tanzania, Sheikh Simba Shaaba (kushoto), Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, Waziri Mkuu mstaafu na Makamu Mwenyekiti wa CCM mstaafu John Malecela wakimsubiri Mzee Mwinyi kwenye hafla hiyo 
Mzee Mwinyi akikaribishwa kwenye chumba maalum cha mapumziko na viongozi wa taasisi hiyo ya Aga Khan
Mzee Mwinyi akizungyumza na viongozi hao kwenye chumba cha mapumziko
Mzee Mwinyi akizungumza na Makamu  wa Rais wa Taasisi hiyo hapa nchini, Kanal Khimji
Waakiendelea na mazungumzo kwenye chumba cha mapumziko.
Mzungumzo yakiendelea chumba cha mapumziko
Mmoja wa viongozi wa Taasisi hiyo, Altaf Hirani akizungumza na Mzee Malecela ukumbini
Mzee Malecela akiwa na viongozi wa Taasisi hiyo ya Aga Khan
Wageni ukumbini
Wageni ukumbini
Ukumbini
Wageni ukumbini wakimsubiri Mzee Mwinyi
Mzee Mwinyi akiingia ukumbini na Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam
Mzee Mwingi akiketi meza kuu
Mzee Mwinyi akiwa ameketi meza kuu na viongozi wa Tasisi hiyo ya Aga Khan
Sheikh Mkuu, Muft wa Tanzania akiingia ukumbini
Makamu wa Rais wa Taasisi ya Aga Khan Tanzania, Kanal Khimj akitoa manano ya utangulizi kabla ya kumkaribisha Mzee Mwinyi kuzungumza
Mzee Mwinyi akizungumza
"Hekima ikiongezeka Maneno yanapungua", akisema Mzee Mwinyi mwishoni mwa hotuba yake iliyojaa hekima. Imetayarishwa na theNkoromo Blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages