Breaking News

Your Ad Spot

Feb 15, 2014

TRANSEVENTS MARKETING WASHEREHEKEA VALENTINE’S DAY KWA KUHIMIZA USALAMA KWENYE VYOMBO VYA USAFIRI

Meneja Uhusiano wa Transevents Makerting, Ednah Rebeccah akitoa maelezo kwa washindi wa shindano la Dereva Makini Sabreena Munir na Vincent Bern ambao walipatikana kwa kujibu maswali kupitia ukurasa wa facebook wa kampuni hiyo yaliyolenga kujua ufahamu wao katika kuzingatia usalama kwenye vyombo vya usafiri.
 
 Mshindi wa shindano la 'Maswali ya Usalama Barabarani' Sabreena Munir akipokea kuponi ya kwenda kula chakula cha usiku kwenye mgahawa wa Akemi unaozunguka (Akemi revolving restaurant)
 Mshindi wa shindano la 'Maswali ya Usalama Barabarani' Vincent Bern akipokea kuponi ya kwenda kula chakula cha usiku kwenye mgahawa wa Akemi unaozunguka (Akemi revolving restaurant)

 Meneja Uhusiano wa Transevents Makerting, Ednah Rebeccah akitoa maelezo kwa washindi wa shindano la Dereva Makini Sabreena Munir na Vincent Bern ambao walipatikana kwa kujibu maswali kupitia ukurasa wa facebook wa kampuni hiyo yaliyolenga kujua ufahamu wao katika kuzingatia usalama kwenye vyombo vya usafiri.
 Washindi hao wamepata zawadi ya chakula cha usiku wakiwa na wenza wao kwenye mgahawa Akemi unaozunguka (Akemi revolving restaurant), pamoja na vinywaji na usafiri.

Meneja Uhusiano wa Transevents Makerting, Ednah Rebeccah anasema lengo la kutoa shindano hilo siku ya wapendanao ni kuihimiza jamii kuitumia siku hiyo kwa kukumbushana mambo ya usalama barabarani.

Anasema kuwa ajali za mara kwa mara zinazotokana na kutozingatiwa kwa sheria za usalama kwenye vyombo vya usafiri zimechukua maisha ya watu wetu wa karibu na wapendwa wetu.

“Ni vyema kutumia siku hii kukumbushana namna ya kuzingatia usalama kwenye vyombo vya usafiri, ni vyema kuhakikisha unazingatia usalama maana kusafiri na kufika salama uendako ni zawadi kubwa sana ya Valentine” anasema Edna

Transevents Marketing imeanzisha kampeni ya dereva makini ambayo inalenga kuhamasisha madereva nchini kuendesha kwa kufuata sheria za barabarani na kuwa makini katika uendeshaji wao.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages